Mzee mmoja shabiki sugu wa Liverpool alinyanyuka na kutoka uwanjani. Akasogea hadi ‘Pub’ iliyokuwa jirani, akaagiza glasi ya ‘Whisky’ kupooza koo lake lililokuwa linaungua moto, kisha akawasha sigara kutuliza mapafu yake yaliyokuwa yakiumia kwa kukosa hewa. Alipomaliza akashika njia na kurudi uwanjani.
Aliiendea siti yake kisha akanyanyua mikono yake juu na kuishusha chini. Akarudia tena mara ya pili na ya tatu, kisha jirani yake wa kulia na kushoto wakamfuata. Dakika mbili mbele jukwaa zima lilimfuata. Taratibu akaanzisha ‘goma’ la ‘Fields of Anfield Road’. Hapo ndipo mashabiki wa Liverpool walivaa ule ukichaa wao halisi. Wakaimba kwa hisia kali sana. Hadi waturuki na ukichaa wao waliwashangaa. Yaani mpo nyuma tatu kwa bila halafu mnaimba hivi?
Kule chumbani Rafael Benitez alimaliza kutoa maelekezo. Kisha akamuachia Steven Gerrard amalize kabla hawajarudi kipindi cha pili. Gerrad alisimama katikati ya chumba akasema, “Hapa sizungumzi kama captain, bali nazungumza kama shabiki wa kutupwa wa Liverpool. Mnawasikia hao wanaopiga hizo kelele? Wamesafiri kwa basi hadi kufika hapa, wamechoka, hawajalala toka jana. Tumeshafungwa tatu lakini bado hawajakata tamaa. Hao ndio Liverpool. Twendeni tukailipe imani yao kwetu. Hata ikibidi tuiache miguu uwanjani. Sisi ndio Liverpool. Tunaweza.”
Waliporejea kipindi cha pili, Benitez akafanya mabadiliko. Akamtoa Steve Finnan na kumuingiza Dietmar Hamman. Liverpool wakatoka kwenye 4-4-1-1 na kuingia 3-5-2. Hapo ndipo balaa lilipoanzia. Kumbuka kule jukwaani goma la fields of Anfield linaendelea kungurumisha.
Hapo ndani anatajwa ‘mr. Liverpool’ Billy Shanky na masikitiko ya kifo chake. Anatajwa Bob Paisley na maajabu ya Roma ya mwaka1977, anatajwa Kenny Daglish na heshima yake. Inapofika hapo haiwi soka tena bali mapambano ya uhai na kifo. Kila mchezaji wa Liverpool anakuwa radhi kupasuka kichwa, kutoka macho na kuvunjika mguu kwa ajili ya Liverpool, hisia zinakuwa kali sana.
Ndipo hapo dakika ya 54 John Riise anamimina krosi inaishia kichwani mwa Gerrard. Ndipo hapo dakika ya 56…
ITAENDELEA…
Naam, hapa ni mahali pako! Kuwa shujaa kwenye sloti hii ya Samurai Ken ujishindie mkwanja na kujipa burudani murua.
Amiri Kayera
Liverpool walifanya comback ya hatarii
Issa
This is anfield
Sylvester
Makala nzui bora uhondo ungeisha leo leo
felister
hii ndio Liverpool
Dorophina
Kikosi cha Liverpool kipo vizuri sana
Lydia Emmanuel Magoti
Naikubali Liverpool wakiamua kufanya yao washindwagi
Adelta
Hii Ni bonge la makala
Venerose
Liverpool wapo vinzur
Sauda
Liverpool wamejipanga
Caroline
Hao ndo mashabiki kindakindaki
Fatina mfingi
Liverpool club kubwa naikubali hatar
Angelina
Safi
Mwajumah
Liverpool iko vizuri sana
Shani
Nice
Tatu
Liverpool wapo vizuri
aisha
Liverpool safi sana
Fatuma kasomo
Gud news
Ernest
Liverpool wazee wa kupindua Meza
Sabrina
Liverpool tishio
David Pere
Yalikuwa maajabu kweli kweli
Janeflora malisa
Good
magdalena
liverpool walifanya kazi kubwa sana
Saupha mohamed
Good news
zeiyana
liverpool wapo vizuri
Hopemwaikuka
Hii ndio liverpool
Povel
Mambo ni moto