Fowadi wa Paris Saint-Germain Kylian Mbappe amekiri kwamba bado hana uhakika na hatma yake wakati ya mazungumzo ya mkataba na mabingwa wa Ufaransa yakiendelea.
Nyota huyo wa zamani wa Monaco anaendelea kuhusishwa na uhamishaji wa mkwanja mrefu kwenda Liverpool au Real Madrid, wakati mkataba wake wa Parc des Princes unakamilika msimu wa joto wa 2022.
Mbappe amebainisha kuwa mazungumzo yanaendelea kuhusu makubaliano mapya, lakini pia amethibitisha kuwa bado hatasaini makubaliano mapya aliendelea kufanya tathmini.
Akizungumza na waandishi wa habari baada wiki iliyopita baada ya ushindi dhidi ya Montpellier HSC, Mfaransa huyu aliyeshinda Kombe la Dunia alisema: “Niko katika kipindi cha kutafakari.
“Nataka kujua ninachotaka katika miaka michache ijayo – wapi nataka kuwa. Nina furaha hapa, lakini sitaki kusaini mkataba na kuondoka mwaka mmoja baadaye.”
Magoli mawili ya Mbappe katika ushindi dhidi ya Montpellier kumemfikisha hadi magoli 14 ya ligi kwa msimu huu, lakini PSG inaeleweka kuwa wapo tayari kwa kumuuza msimu huu wa joto ikiwa hatatoa hatma yake kwa klabu.
Anayejaribu hawezi kutoka kapa Meridianbet! Kasino ya mtandaoni ya Meridianbet inakuhakikishia ushindi mkubwa kila unapojaribu kuingia mchezoni. Washindi hushindana, ingia mchezoni!
Adelta
Monaco ni mtu makini Sana
Khadija
Itakuwa sasa
Venerose
Asijal Mambo yatakuwa manzur
Sania
Mbappe atulize kichwa
Caroline
Mbappe bado hajakubali matokeo
Dorophina
Mbappe abakie tu psg
Magdalena
Mbappe wanamzingua tu
felister
mbappe abakie apo apo
Mwanahamisi
Mbappe analia tuu
David Pere
Nyota huyo wa zamani wa Monaco anaendelea kuhusishwa na uhamishaji wa mkwanja mrefu kwenda Liverpool au Real Madrid, wakati mkataba wake wa Parc des Princes unakamilika msimu wa joto wa 2022.
Issa
Ni wakati wa mbape kujiunga nazidane
Ernest Kimeru
Hapa mchawi ni Real Madrid kwani ndio wanamuwinda Mbappe
Hopemwaikuka
Uamuz ni wako
warda
Atajua tu