Mbappe: Kubakia PSG Pesa Sio Sababu

Mshambuliaji wa klabu ya PSG Kylian Mbappe amesema kuwa kitendo cha yeye kuamua kubaki kwenye timu hiyo hakijachagizwa na pesa bali ni mazungumzo ya maendeleo ambayo klabu hiyo inataka kufanya.

Mbappe ameweka wazi kilichomfanya akubali kusali kwenye klabu ya Paris Saint Germain licha ya kufanya makubaliano ya mdomo na rais wa klabu ya Real Madrid Florentino Perez, wakati akihojiwa alinukuliwa akisema.

Mbappe
Kylian Mbappe

“Tumezungumza kwa mwezi sasa na mkuregenzi wa michezo kuhusu miradi ya maendeleo ya soka na tumetumia muda mchache sana kuzungumzia pesa.

“Kila mtu alifahanu kuwa nilikuwa nataka kuondoka mwaka uliopita. Nilijishawishi kuwa huo ni uamuzi bora kwa kipindi kile. Muktadha ni tofauti sasa, kwenye mchezo na vigezo binafsi.

“Mimi natokea nchi ya Ufaransa, sehemu ambayo nataka kuishi, kuzeekea na kuamalizia maisha yangu ya soka. Kuondoka haikuwa sawa ni rahisi kuweza kupumbazika kwenye hili, hii ni nchi yangu.

“Mradi wa soka unakwenda kubadilika, klabu inataka mabadiliko na naamini hadithi yangu bado haijaisha , kuna kurasa nahitaji kuziandika bado.”


TENGENEZA FAIDA NA ZEUS ANCIENT FORTUNES

Una Kila sababu ya kufurahia wiki yako na kutengeneza mwaka huu uwe wa faida zaidi katika kasino zetu za mtandaoni za meridianbettz. Mchezo wa Zeus Ancient Fortunes unakuongoza kutekeleza hilo.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe