Tanguy Ndombele: Nilihitaji Kitu Kingine Zaidi

Tanguy Ndombele amekubali kuwa alipata msongo akiwa kwenye klabu ya Tottenham baada ya kuwa chini ya makocha watano pasipo muendelezo wowote na hakuhitaji kuona mwisho wake ukiwa ndani ya klabu hiyo.

Ndombele alieleza jinsi ambayo hali hiyo ilivyomuathili kwa kutokuwa na muendelezo mzuri baada ya klabu hiyo kuwa chini ya makocha watano ambao Mauricio Pochettino, Jose Mourinho, Ryan Mason, Nuno Espirito Santo na Antonio Conte.

Hailikuwa kosa lao lakini nilikuwa na tatizo kidogo nikiwa Tottenham, nilikuwa nataka kitu kingine zaidi.

Tanguy Ndombele

Alipohojiwa  na kituo cha RMC Sport, alinukuliwa akisema, “sikusita klabu ya Lyon ilipoonesha nia ya kunihitaji, mazungumzo yalikuwa haraka, nina furaha kurudi, najua lyon ni wazuri kuendana mazingira, nina miezi mitatu na nusu kabla ta msimu kuisha, Lyon sio sehemu mbaya kwangu.”

Ndombele alivunja rekodi ya usajiri kwenye klabu ya Tottenham mwaka 2019 lakini hakuwa na msimu mzuri kwenye kikosi cha timu hiyo, kwenye misimu miwili na nusu aliyoitumikia klabu hiyo.


VUNA MKWANJA NA KENO

Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.

tetesi, Tetesi za Soka barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe