Kiungo mkabaji wa kimataifa wa Brazil, Casemiro, amesema sababu kubwa iliyomshawishi kujiunga na Inter Miami CF ni kutimiza ndoto ya kucheza pamoja na nyota wa Argentina, Lionel Messi.
Casemiro mwenye umri wa miaka 34 alitambulishwa rasmi na Inter Miami siku ya Alhamisi baada ya kujiunga na klabu hiyo ya Ligi Kuu ya Marekani (MLS) kama mchezaji huru, kufuatia kuondoka Manchester United mwishoni mwa msimu uliopita.
mpira wa miguu, kubeti mpira wa miguu, bashiri soka, soka, beti kwenye soka, odds za soka, bashiri mpira wa miguu, beti za soka, beti mechi za soka, odds za kubeti mpira wa miguu
Akizungumza na waandishi wa habari katika mkutano wa utambulisho wake, kiungo huyo alisema uamuzi wake haukutokana na fedha wala changamoto mpya, bali hamu ya kucheza sambamba na Messi na kumsaidia kuendelea kushinda mataji.
Casemiro alieleza kuwa anajivunia kuwa sehemu ya kikosi cha Inter Miami na anaamini uzoefu wake utasaidia timu hiyo kufikia mafanikio zaidi, huku akisisitiza kuwa Messi ni mmoja wa wachezaji wakubwa zaidi kuwahi kutokea katika historia ya mchezo wa soka.
“Kwangu mimi, bila shaka yoyote niko hapa ili tu kucheza na mchezaji bora zaidi wa muda wote, Lionel Messi. Nataka kufurahia hali hiyo na kumsaidia kuendelea kushinda, kwa sababu yeye ni mshindi. Niko mahali ninapotaka kuwa. Niliondoka Manchester United kama mchezaji huru. Nataka kufurahia kuwa naye, kumsaidia kushinda na kumfanya awe mkubwa zaidi. Yeye ni mmoja wa magwiji au tuseme ‘Mungu’ wa soka na nataka kutoa mchango wangu kwake,” amesema Casemiro.


