Lionel Messi Afunga Bao Mbili, Inter Miami Ikiifunga FC Cincinnati

Nahodha wa Argentina, Lionel Messi ameonyesha kiwango cha juu baada ya kufunga mabao mawili na kusaidia mengine mawili, akiiongoza Inter Miami CF kushinda 5-3 dhidi ya FC Cincinnati katika mchezo wa Ligi Kuu ya Marekani (MLS) uliochezwa ugenini.

Lionel Messi Afunga Bao Mbili, Inter Miami Ikiifunga FC CincinnatiKwa matokeo hayo, Inter Miami imeendelea kuimarika msimamo wake katika Kanda ya Mashariki ikiwa na pointi 25, huku Messi akiendelea kuwa katika kiwango bora kabla ya Kombe la Dunia linalotarajiwa kufanyika Amerika ya Kaskazini.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Messi alifungua ukurasa wa mabao dakika ya 24 baada ya kufuatilia mpira uliotokana na makosa ya beki Matt Miazga, kisha Cincinnati kusawazisha kupitia penalti ya Kevin Denkey dakika ya 41, na kwenda mapumziko sare ya 1-1.

Lionel Messi Afunga Bao Mbili, Inter Miami Ikiifunga FC CincinnatiBaada ya mapumziko, Cincinnati walitangulia tena kupitia Pavel Bucha, lakini Messi alirejesha matumaini ya Inter Miami kwa kufunga bao la kusawazisha dakika ya 55 kwa shuti kali la mguu wa kushoto akimalizia pasi ya Rodrigo De Paul.

Cincinnati waliendelea kupambana na kurejea mbele kupitia Evander dakika ya 64, lakini Inter Miami walipata mabao mengine kupitia Mateo Silvetti pamoja na mchezaji wa Mexico German Berterame kabla ya Messi kuhusika tena kwenye bao la mwisho dakika ya 89, ambapo shuti lake liligonga mwamba na kumgonga kipa Roman Celentano na kuwa bao la kujifunga.

Lionel Messi Afunga Bao Mbili, Inter Miami Ikiifunga FC CincinnatiKocha wa Inter Miami, Guillermo Hoyos, aliisifu timu yake akisema “Walichofanya leo kilikuwa cha kuvutia dhidi ya timu ngumu na kwenye uwanja mgumu. Ni vigumu sana kucheza hapa.”

Lionel Messi Afunga Bao Mbili, Inter Miami Ikiifunga FC CincinnatiAliongeza “Ni wazi kwamba hawapo MLS kwa matembezi tu. Wapo hapa kucheza, kutoa kila kitu, na kuonyesha dunia kwamba soka linachezwa hapa pia. Tunaondoka tukiwa na furaha kubwa. Tulicheza kiwango cha juu sana cha soka.”

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.