Kiungo wa timu ya taifa ya Scotland Scott McTominay amepewa heshima ya kipekee baada ya bao lake la kuvutia dhidi ya Denmark kuwekwa kwenye noti maalum ya pauni 20 iliyozinduliwa na Bank of Scotland kwa ajili ya kuadhimisha kurejea kwa Scotland katika Fainali za Kombe la Dunia baada ya miaka 28.
McTominay aliingia kwenye historia ya soka la Scotland baada ya kufunga bao la kubinuka (overhead kick) katika ushindi wa mabao 4-2 dhidi ya Denmark kwenye mchezo wa mwisho wa kufuzu Kombe la Dunia 2026 uliochezwa Novemba 18, 2025. Bao hilo lilifungwa katika dakika ya pili ya mchezo na kusaidia Scotland kuongoza Kundi C pamoja na kufuzu rasmi kwa michuano hiyo itakayofanyika Marekani, Mexico na Canada.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa mujibu wa Benki ya Scotland, noti hizo maalum ni 100 pekee zilizochapishwa, huku 50 kati yake zikitarajiwa kupatikana kupitia mnada wa wakusanyaji, droo za zawadi pamoja na “vaults” maalum zitakazowekwa katika miji ya Glasgow na Edinburgh.
“Bao lile limekuwa sehemu ya historia ya taifa letu na lilistahili kuenziwa kwa njia ya kipekee,” ilieleza taarifa ya Benki ya Scotland wakati wa uzinduzi wa noti hizo maalum zinazomuenzi McTominay kwa mchango wake mkubwa kwa taifa hilo.
Aidha, sehemu ya mapato yatakayopatikana kutokana na noti hizo maalum yataelekezwa kwa Crisis Scotland, taasisi inayosaidia watu wasio na makazi nchini Scotland, huku mashabiki wengi wakielezea hatua hiyo kama kumbukumbu muhimu ya mafanikio ya timu yao ya taifa.


