Neymar Awasili Kambi Ya Brazil Kwa Chopa, Ahofiwa Kukosa Mechi Ya Morocco

Mshambuliaji nyota wa timu ya taifa ya Brazil, Neymar Jr, amewasili kambini nchini Marekani kwa mtindo wa kipekee baada ya kutumia helikopta maarufu kama ‘Chopa’, tayari kwa maandalizi ya michuano ya Kombe la Dunia 2026.

Neymar Awasili Kambi Ya Brazil Kwa Chopa, Ahofiwa Kukosa Mechi Ya MoroccoBrazil imeweka kambi katika kituo cha Columbia Park Training Facility kilichopo Morris Township, New Jersey, ambacho hutumiwa pia na klabu ya New York Red Bulls ya Ligi Kuu Marekani (MLS).

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Kuwasili kwa staa huyo kulizua gumzo kubwa kambini hapo huku akipokelewa kwa furaha na kocha mpya wa Brazil, Carlo Ancelotti, pamoja na wachezaji wenzake waliokuwa tayari wameanza mazoezi tangu mapema wiki hii. Mashabiki waliokuwa eneo hilo walionekana kuvutiwa na namna Neymar alivyoingia kambini kwa usafiri huo wa kifahari.

Neymar Awasili Kambi Ya Brazil Kwa Chopa, Ahofiwa Kukosa Mechi Ya Morocco“Tunafurahia kumuona Neymar akiwa sehemu ya kikosi, uwepo wake unaongeza morali kubwa kwa timu,” kilieleza chanzo cha karibu na benchi la ufundi la Brazil baada ya kuwasili kwa mshambuliaji huyo mwenye uzoefu mkubwa katika michuano ya kimataifa.

Neymar Awasili Kambi Ya Brazil Kwa Chopa, Ahofiwa Kukosa Mechi Ya MoroccoHata hivyo, taarifa kutoka kambini zinaeleza kuwa Neymar hataanza mazoezi mazito mara moja kutokana na kusumbuliwa na jeraha dogo la misuli ya paja. Madaktari wa timu hiyo wameendelea kufanya vipimo zaidi vya kitabibu ili kufuatilia maendeleo ya nyota huyo kabla ya kumpa ruhusa ya kurejea kwenye mazoezi ya kawaida.

Neymar Awasili Kambi Ya Brazil Kwa Chopa, Ahofiwa Kukosa Mechi Ya MoroccoKutokana na hali hiyo, kuna uwezekano mkubwa wa Neymar kuukosa mchezo wa kwanza wa ufunguzi wa Kombe la Dunia 2026 ambapo Brazil itachuana na Morocco. “Hatutaki kufanya haraka kuhusu afya yake, muhimu ni kuhakikisha anakuwa fiti kwa mechi zinazofuata,” kiliongeza chanzo hicho huku mashabiki wa Brazil wakisubiri kwa hamu taarifa rasmi kuhusu hali yake.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.