Nguli wa soka wa England, Ian Wright, ameibua mjadala mkubwa baada ya kukosoa changamoto mbalimbali zinazojitokeza kuelekea michuano mikubwa ya 2026 itakalofanyika Marekani, Canada na Mexico. Wright amesema hali inayoendelea inaonyesha dalili za sintofahamu ambazo zinaweza kuathiri maandalizi ya michuano hiyo mikubwa duniani.
Wright alizungumza kufuatia taarifa za mwamuzi wa Somalia, Omar Abdulkadir Artan, kunyimwa ruhusa ya kuingia Marekani licha ya kuwa miongoni mwa waamuzi waliopangwa kushiriki katika michuano hiyo. Tukio hilo limeibua mjadala mpana kuhusu vikwazo vya uhamiaji vinavyoweza kuathiri washiriki wa mashindano.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Amesema kuwa changamoto hizo zinaongeza orodha ya matukio yanayowahusisha mashabiki, wachezaji, maofisa na waandishi wa habari wanaokumbana na vikwazo vya kusafiri. Wright alisisitiza kuwa “hii siyo tu suala la michezo, bali ni suala la haki na usawa kwa kila anayehusika katika mashindano.”
Kwa upande wake, Shirikisho la Soka la ulimwenguni limethibitisha kuwa Artan hataweza kushiriki kwenye michuano hii mikubwa baada ya kuzuiwa kuingia Marekani alipowasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Miami. Msemaji wa shirikisho hilo Bryan Swanson, amesema “Shirikisho halina mamlaka ya kuingilia maamuzi ya ndani ya nchi kuhusu masuala ya uhamiaji.”
Wright ameonya kuwa hali hiyo inaweza kuharibu taswira ya mashindano hayo, akiyaita “mashindano yasintofahamu.” Amelitaka shirikisho na nchi wenyeji kuchukua hatua za haraka kuhakikisha washiriki wote wanapata fursa sawa bila vikwazo vinavyoweza kuathiri mafanikio ya tukio hilo kubwa la kimataifa.


