Kocha wa timu ya taifa ya Hispania, Luis de la Fuente, ametangaza kikosi cha nchi hiyo kitakachoshiriki Kombe la Dunia 2026 huku kinda nyota wa FC Barcelona, Lamine Yamal, akijumuishwa licha ya kuwa na majeraha ya misuli ya paja.
Yamal mwenye umri wa miaka 18 amekuwa nje ya uwanja tangu mwishoni mwa Aprili baada ya kupata majeraha akiwa na Barcelona, hali inayotia mashaka ushiriki wake katika mechi za mwanzo za mashindano hayo. Hata hivyo, kocha De la Fuente ameonyesha imani kubwa kwa nyota huyo aliyeng’ara kwenye michuano ya Euro 2024.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kiungo wa Arsenal F.C., Mikel Merino, naye amerejea kikosini baada ya kupona jeraha la mguu lililomuweka nje tangu Januari. Merino alicheza kama mchezaji wa akiba katika mchezo wa mwisho wa Ligi Kuu England dhidi ya Crystal Palace F.C.
Kwa mara ya kwanza katika historia ya Kombe la Dunia, kikosi cha Hispania hakitakuwa na mchezaji yeyote kutoka Real Madrid CF. Beki Dean Huijsen ameondolewa, huku mkongwe Dani Carvajal naye akikosa nafasi kutokana na msimu uliokumbwa na majeraha.

Kocha huyo pia amewajumuisha mabeki Eric Garcia na Marc Pubill baada ya kuwa na misimu mizuri katika klabu zao, huku Robin Le Normand akiachwa nje ya kikosi.
Winga wa Athletic Club, Nico Williams, ambaye alikuwa muhimu katika ushindi wa Euro 2024 pamoja na Yamal, pia ameitwa licha ya kusumbuliwa na matatizo ya utimamu wa mwili msimu huu.


