Al Hilal imeanzishwa 1930 ikiwa ni mabingwa mara nyingi zaidi wa ligi juu nchini Sudan ikiwa ikiwa imebeba ubingwa huo mara 29, ubingwa wa kwanza walibeba 1965 huku wa 29 wakibeba 2022.
Wakiwa chini ya kocha Florent Ibenge wamefanikiwa kuwatoa Saint Goerge kwa agg ya bao 2-2 wakinufaika na bao 1 la ugenini.
Al Hilal wanatumia uwanja wao uliopo Omdurman Khartoum ukiwa na uwezo wa kuingiza mashabiki 25,000.
Idadi kubwa ya kikosi chao kinaundwa na wachezaji wandani, wakiwa na wachezaji 9 tu raia wa kigeni kutoka mataifa ya Senegal, Ghana, Cameroon, Angola, Congo Nigeria na Malawi.Hawa wamewahi kucheza fainal mbili za CAF CL.
Ni wakati wa wananchi kuonesha ukubwa wao barani Afrika kwasababu historia zipo kwa ajili ya kuvunjwa.
Kwa habari na matukio ya kimichezo na ya uhakika tembelea Youtube channel yetu Meridian Sport