David Beckham anasema kucheza na Kylian Mbappe “ingekuwa ndoto” baada ya supastaa huyo wa Paris Saint-Germain kupachika bao lake la 100 kwa klabu.
Mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 21, aliyejiunga na PSG kutoka kwa wapinzani wao wa nyumbani Monaco mwezi Agosti 2017, alifikia hatua hiyo kwenye mchezo dhidi ya Montpellier siku ya Jumamosi.
Amefikisha magoli karne katika ya michezo 137 tu na rekodi nyingi zaidi zitafuata kwa mshindi wa Kombe la Dunia.
Beckham, ambaye alimaliza taaluma yake katika klabu ya PSG mwaka 2013, anatamani angekuwa bado anacheza na kuweza kumsaidia Mbappe kufukuza mfungaji wa rekodi ya muda wote Edinson Cavani (200)
Nahodha huyo wa zamani wa England alifunga goli mbili na kutengeneza asisti sita katika michezo yake 10 ya Ligue 1 (dakika 311 alicheza), lakini Mbappe pia anaweza kuwa ameboresha takwimu zake mwenyewe.
“Ningependa bado kuwa mchezaji, kwa sababu kucheza na fowadi kama Kylian ingekuwa ndoto kwangu,” mmiliki wa Inter Miami Beckham aliiambia Telefoot.
“Unaweka mpira mahali popote mbele yake na anaupata.”
Mbappe ameweka wastani wa bao kila dakika 89 kwa PSG kwenye Ligue 1, akifunga 74 kati ya mabao yake 100 kwenye mashindano hayo.
Kulikuwa na mengine 13 kwenye Ligi ya Mabingwa, ingawa mshambuliaji huyo hajafunga katika mashindano ya Ulaya msimu huu 2020, hata wakati PSG ilifika fainali ya msimu uliopita.
Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!
[email protected]
Kigezo ni umri isingewezekana
Zahara Omary
Duuh
samiah
Duuh
Neema
Kucheza nae mbona inawezekana
Magdalena
Umri tu wa Beckham ndo ushaenda ila ingewezekana
Devotha
Kucheza nae ingewezelana
warda
Beckham anapenda sana kucheza na watu maarufu sema ndo hivyo mda ushapita
Rahma
Ingewezekana tu kucheza nae
Fatina mfingi
Mbona rais tyu
Fatuma kasomo
Itakua poa tu
Lydia Emmanuel Magoti
Ingewezekana tuuu kwasababu mbappe anauwezo wakucheza timu yoyote hile
Tatu
Mbona inawezekana
Adelta
Inawezekana yeye tu
Ernest
Mbappe ni mchezaji nyota ajae baada ya Messi na CR7 kupotea kwenye soka
Sarah
Inawezekana mbona
Janeflora malisa
Dah
Dorophina
Bekham umri umeshaenda isingewezekana
Hopemwaikuka
Imeisha hyoo
Issa
Beckham ametikisa sana enz zake na alikua kiungo muhimu sana england
Saupha mohamed
Beckham alikua MTU mbaya
Theckla
Hatari
Sabrina
Ingependeza sana tatizo muda Beckham wakati ukuta