Benzema Hati Hati Kuwakosa Bilbao, PSG.

Mshambuliaji wa Real Madrid, Karim Benzema huenda akaukosa mchezo Robo Fainali wa Copa del Rey na ule wa Hatua ya 16 Bora wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya PSG, baada ya kuumia wikiendi hii wakati wakicheza dhidi ya Elche.

 

Benzema aliumia katika mchezo huo ambao ulimazilika kwa sare ya 2-2 na nafasi yake ikachukuliwa na Luka Jovic. Mchezaji huyo anatarajiwa kufanyiwa vipimo vya Ultrasound kujua tatizo lake lina ukubwa kiasi gani.

Taarifa zinaeleza kuwa nyota huyo atakuwa nje kwa siku 8 mpaka 10 na kwa maana hiyo mchezo dhidi ya Bilbao wa Copa del Rey anaweza kukosekana na ule dhidi ya PSG.

Kwa maana hiyo, Madrid katika mchezo huo wa Copa del Rey itamkosa Benzema, Eder Militao, Vinicus Junior, Rodrygo Goes na Casemiro hawa watakuwa timu ya Taifa ya Brazil na watamkosa pia Federico Valverde (Uruguay) na nahodha wao Marcelo.


VUNA MKWANJA NA KENO

Dakika tano pekee zinakutosha kuwa mmoja wa washindi wa mkwanja mrefu ndani ya kasino pendwa ya meridianbettz katika sloti maridhawa ya KENO, moja ya michezo inayoipa thamani dau lako.

tetesi, Tetesi za Soka barani Ulaya., Meridianbet

CHEZA HAPA

Acha ujumbe