Chelsea Kuendelea Kuvaa Nembo ya 'Three' 3

Klabu ya Chelsea itaendelea kuvaa nembo ya 3 kwenye jezi zao  licha ya kampuni hiyo kusitisha udhamini wa £40milion mwaka kutokana na klabu hiyo kuwekewa vikwazo na kampuni ya Nike kutoruhusiwa kuwatengenezea vifaa vipya.

Kampuni hiyo ya mawasiliano ilisitisha udhamini wake wenye thamani ya £40million, siku ambayo mmiliki wa klabu hiyo aliwekewa vikwazo na kuitaka klabu ya Chelsea kuondoa nembo yao kwenye jezi zao haraka iwezekanavyo.

 

Lakini ombi lao halijaweza kufanikiwa, chini ya kibali maalim ambacho klabu ya Chelsea imepewa kwa ajiri ya uendeshaji wa klabu hiyo hakiruhusu mtengenezaji wa jezi kuweza kuwatengenezea jezi nyingine mpya, haruhusiwi.

Chelsea wametumia jezi zenye nembo ya 3 kwenye michezo minne tangia Abramovich awekewe vikwazo, kwenye kipindi hichi cha mapumziko ya kimataifa wamejaribu kutatua hili tatizo lakini imeshindikana, walikuwa na mpango wa kuzipaka rangi sehemu yenye nembo ya 3 lakini wamekatiliwa.

Mdhamini mwingine aliyejitoa ni Hyundai ambaye nembo yake ilikuwa mikononi lakini hawakuomba nembo yao itolewe.


3500 NI YAKO UKIJIUNGA TU MERIDIANBET!

Una nafasi ya kupata bonasi ya shilingi 3500 kwa ajili ya kuanza safari yako ya kasino ya mtandaoni ya Meridianbet.

Kubeti Poa - Bonasi Kubwa

Jisajili sasa

Acha ujumbe