De la Hoya Anaamini Garcia Atamzidi Canelo kwa Ukubwa

Oscar De la Hoya alifunguka siku ya Ijumaa kwamba bondia Ryan Garcia atampita Canelo Saul Alvarez kwa ukubwa siku za badaye.

De la Hoya Anaamini Garcia Atamzidi Canelo kwa Ukubwa

Uhusiano wa De la Hoya uliingia dosari tangu wawili hao waache kufanya kazi pamoja hivyo Hoya kutomuongelea vizuri Canelo ni jambo la kawaida na ikumbukwe Ryan Garcia aliachana na Gym ya Canelo baada ya Caneolo kudai kwamba Garcia hana umakani na kazi yake na anapoteza muda wake.

De la Hoya anaongea hayo zikiwa zimepita wiki 3 tu tangu alipoteza mikononi mwa Dmitry Bivol wakati Ryan Garcia anatafuta ushindi wa 23 mfululizo.

De la Hoya, pia anatambua kwamba mwanafunzi wake Garcia lazima atulize kichwa  chake na kukaa kwenye njia sahihi bila usumbufu wowote ili kupita mafanikio ya Canelo.

“Ninaamini kwamba Ryan Garcia, kwa umakini katika ndondi, anaweza kufanikiwa. Hakuna cha kumzuia,” De la Hoya alisema katika mahojiano na David Faitelson wa ESPN.

“Atakuwa jambo la ajabu, atakuwa mkubwa kuliko Canelo Alvarez.

“Nilipokuwa nikimpandisha Canelo kutoka pambano lake la kwanza hapa Marekani dhidi ya Larry Mosley, hakuwa na mtandao wa kijamii, hakuwa na umaarufu, hakuwa Marekani.


ALIYA’S WISHES

Bila shaka unatamani ushindi mkubwa, vipi kuhusu kujaribu Sloti hii ya Aliya’s Wishes? jaribu ushinde sasa.Kasino ya Mtandaoni

CHEZA SASA

Acha ujumbe