Leo hii kuna maamuzi magumu yanatarajiwa kuchukuliwa kwa maslahi ya Barcelona mpya wengi wakitaka Rais Josep Maria Bartomeu ajiuzulu wadhfa wake.
Kiongozi wa vuguvugu hilo Durch Marc anasimamia msimamo kuwa bodi inapaswa kutoa majibu leo kama wanajiuzulu au waruhusu kura za kuamua hatma (vote of censure)
Inaaminika Bartomeu yupo tayari kujiuzulu ila anasubiri muongozo kutoka Mahakama ya kimichezo ya jimbo la Catalunya, huku pia Marc na wenzie wanataka kuipeleka kesi huko kama leo Bartomeu hatotoa majibu ya kuridhisha.
Katika hatua nyingine, wachezaji wa Barcelona Kupitia njia ya Burofax, walitoa taarifa ya kuhudhuria kikao cha leo kuhusiana na maamuzi ya kupunguzwa mishahara yao, lakini inasemekana wamegoma kurejea mezani kuzungumzia suala hilo.
Barcelona atakutana na timu ya Pirlo Juventus katika michuano ya Champions League huku ikiwa na kumbukumbu ya maumivu katika LaLiga kwa kuchapwa bao 3-1 na mahasimu wao Real Madrid, Je Barca wataendelea kusuasua? Usiache kufanya ubashiri wa mechi hii ndani ya Meridianbet tembelea tovuti www.meridianbet.co.tz.
Tunazungumzia mkwanja wa Tshs.160,000,000! Kupitia Kasino ya Mtandaonii ya Meridianbet unaweza kuwa milionea wakati wowote.
Dorophina
Hapo kwa Barca ni bora wapige kura za maoni
Hopemwaikuka
Dah !
aisha
Poleni sana barcelona kwa majanga
Sauda
Barcelona hawana jipya.
Fatina mfingi
Daaah mbona majanga
Mwajumah
Poleni sana barcelona
Lydia Emmanuel Magoti
Duu Barcelona ngoma ngumu
Tatu
Bora ajiuzulu
Ester jackson
Ajihuzulu tu inatosha alivyoitumikia timu hiyo
Sabrina
Duuh noma sana
Elika
Pole sana
warda
Duu kama Simba
Ernest
Ngoja tuone, mchawi atagundulika tuu
Povel
Hapo ndo wakat wa kushikana masharti ndani ya nou camp