Neviile Southall anaamini Kepa Arrizabalaga na David de Gea wanatakiwa kujifunza suala la thamani kutoka kwa Bingwa wa dunia katika maswala ndondi uzito wa mkubwa Anthony Joshua.
Chelsea walimfanya Kepa kuwa golikipa wa gharama zaidi ulimwenguni mwaka 2018 lakini amekuwa akifanya makosa mara kwa mara yanayo igharimu timu hiyo na kosa la mwisho kufanya ni lile la mchezo dhidi ya Mbaingwa watetezi wa Premier League Liverpool siku ya Jumapili
Kwa sasa wanajiandaa kumpa nafasi ya kwanza golikipa kutoka klabu ya Rennes Edouard Mendy anayetarajia kutua darajani kwa dau linaloripotiwa kufika £22m.
Wakati huo huo mlinda mlango wa Manchester United amekuwa katika wakati mgumu kwa kuwa na kiwango kisicho ridhisha na kocha Ole Gunnar anatarajia kumpa nafasi golikipa Dean Henderson aliyekuwa kwa mkopo katika klabu ya Sheffield United.
Southall ambaye aliisadia timu ya Everton kushinda mataji mawili ya ligi, FA Cup mbili na European Cup Winners’ Cup wakati akiwa Goodison Park, alimpointi mpiganaji Anthony Joshua ambaye alidondoshwa na Andy Ruiz Jr mwezi Juni 2019, lakini alirejesha mkanda wake miezi sita baadaye kuwa funzo kwa magolikipa hao.
“Wakati ukiwa golikipa ukumbuke kila mtu atakuhukumu kama ukiwa umefungwa,’ Southall aliiambia Stats Perform News.
“De Gea aliwahi kudhihirisha kuwa golikipa bora ulimwenguni, lakini kila mtu alianza kupata shaka juu ya kiwango chake kitu ambacho kwangu mimi hakileti maana.
“Ni kama kwa Anthony Joshua alidhihirisha yeye ni bondia bora duniani kwa sababu ameshinda mikanda mingi na kisha kupoteza moja na baadaye alirejesha nadhani kuna funzo kwa Joshua
Aliulizwa anafikiria nini kuhusu kepa akiwa Chelsea Southall alisema: “Wachezaji ni mawaziri wakuu wa soka duniani, kila mtu anawachukia au atawapenda inategemea atawafanyia nini.
FURAHIA KASINO YA MTANDAONI
Tembelea ardhi ya maajabu ushangazwe na mengi ikiwa ni pamoja na urahisi wa kujipatia utajiri kupitia Kasino ya Meridianbet.
Aziza mushi
Asanteni kwa taarifa.
Tumaini kasalile
Wanawangusha sana mafans wao kwa makosa yao yakizembe
Theckla
Sahihi
Ernest
Nimemuelewa sana Southall , Kepa na De Gea wanatakiwa kujifunza kitu hapa lakini binafsi sina shaka na kiwango cha De Gea
magdalena
kepa na mwenzio uwezo wao katika kudaka mpira umeshuka sana wanastahili kujifunza kwa wenzao mbinu mpya
Elika
De gea kiwango chake kipo vizuri sana
Nasra
Yuko vzuri
Shan
Anthony ni mfano wa kuingwa!!
Dorophina
Anthony Ni mfano mzuri inatakiwa wamuige
Lydia Emmanuel Magoti
Kepa na De Gea anatakiwa ajifinze kitu Mimi Kama Mimi sinashaka nae De Gea
Tatu
Hapo Chelsea wamepata hasara bora wamuuze tu huyo goli kipa
Caroline
Kwa kweli kuna la kujifunza.inabidi wapambane kufa na kupona .wanatulet Sana down mashabiki zao
Zeiyana
Me naona mwanzo tu kwa Chelsea wamesajiri wachezaji wengi wenye uwezo imebaki kazi ya kocha tu kupanga wachezaji tunaimani mchezo hunao kuja watafanya vizuri
Neema
Kwa kweliii kepa na De Gea wanahitaji kujifunza kwa anthony ili waimarike vyema.
Sadick
Chelsea ilimununua Kepa bila kutafakari sana kama mbadala wa Thibaut Courtois aliposajiriwa na Real Madrid. Nadhani De Gea atarejea ktk Kiwango chake#meridianbettz
Salma ngende
Nikweli
Gabriel
Chelsea walimfanya Kepa kuwa golikipa wa gharama zaidi ulimwenguni mwaka 2018 lakini amekuwa akifanya makosa mara kwa mara yanayo igharimu timu hiyo na kosa la mwisho kufanya ni lile la mchezo dhidi ya Mbaingwa watetezi wa Premier League Kwa kweliii kepa na De Gea wanahitaji kujifunza kwa anthony
Venerose
Anthony yuko vizuri sana
Janeflora malisa
🔥
jullie
safi sana
Hopemwaikuka
🙊
Hidaya
Yupo vizuri
Ester jackson
Yan kweli kabisa hasa kwa kepa Chelsea walimsajili kwa pesa nyingi lakini ameshindwa kuonyesha dhamani ya pesa yake inabidi awekwe pembeni atafutiwe mwanasaikologia kumjenga kiakili ili arudi kwenye kiwango kizuri mana wachezaji wapo tena wazuri la kipa hamna
Rose kapinga
Anthony wamoto sanaa anajua anachokifanya
Issa
Ni .makipa wazuri sema wana kuwaga wazur kwa msimu tu
lombo
saf
aisha
Anthony yuko vizuri na pia anasitahili pongezi
Amiri Kayera
Kwer kabisa
Rehema
Iko poa
Saupha mohamed
Jamaa yupo vizuri
Sabrina
De Gea yupo vizuri
felister
sahihi
Sauda
Anthony Joshua fundi
Frank P
De gea akafuate changamoto nyingine la sivyo mwisho wake utakuwa mbaya
Latifa juma mohamed
Gud news
farida ahmadi
Kweli kabisah
Mwajumah
Yupo vizur
Samiah
Yupo vzr
David Pere
Nimemuelewa sana Southall , Kepa na De Gea wanatakiwa kujifunza kitu hapa lakini binafsi sina shaka na kiwango cha De Gea