Lampard Ana Nafasi ya Kujifunza Zaidi Nje ya Chelsea.

Ukiniuliza kwanini Frank Lampard msimu uliopita alifanya vema, nitakujibu kuwa, ni kwasababu wachezaji walikuwa wanamtumikia sana. Walikuwa wakimtazama kama ‘role model’ hakuna heshima nyingine ambayo wangeweza kumpa zaidi ya kujitoa kwa ajili yake.

Nakubali kuwa Chelsea ilikuwa inashinda kwa mbinu za Lampard lakini zaidi sana, Chelsea ilikuwa inashinda kwa ari, kujitoa (Spirit). Bahati mbaya ya kushinda kwa ari ni kuwa, timu inapodondora na kuanza kukosa matokeo, huwa inashuka na kupelekea kukosa ujasiri. Ili ari iendelee kuwepo unahitaji kuendelea kupata matokeo.

Lampard Ana Nafasi ya Kujifunza Zaidi Nje ya Chelsea.

Unahitaji nini cha kukupa matokeo zaidi ya mbinu na wachezaji bora? Hakuna. Chelsea kwa sasa wana wachezaji bora. Wanachokosa ni hicho kingine, namna ya kuupata ubora wa wachezaji.

Kupata ubora wa mchezaji unamuhitaji mwalimu zaidi, kisha mchezaji. Mwalimu anaupata ubora wa mchezaji kwa kutengeneza timu ambayo itampa nafasi kila mchezaji kufanya majukumu ambayo yanakuwa bora na marahisi kwake.

Kwa mfano, Kai Haveirtz, si aina ya mtu anayeweza kuwa Mtumwa uwanjani akakimbia kilometa nyingi kuutafuta mpira, si aina ya mtu unayeweza kumtuma akazuie na akafanya vizuri. Ni mpiga pasi mzuri asiyependa bugudha, hivo kama kocha unaitengeneza timu itakayokuwa na watumwa na wafukuza mpira, halafu yeye anafanya kazi yake anayoiweza

Kitu kama hicho unakifanya kwa timu nzima. Wale unaoamua wawe watumwa wanaondoka kwenye majukumu mengine. Inawezekana ukamlazimisha mchezaji kufanya jukumu asiloliweza, lakini unamtengenezea mazingira ambayo atafanya majukumu anayoyaweza zaidi. Labda hiko ndicho kitu anachokikosa Lamps.

Kitu kingine anachokikosa Lampard, ni uvumilivu na kutokujua kipi kinamfaa zaidi. Unajua tofauti na ukuta, labda na Mason Mount katikati ya kiwanja, hakuna wachezaji wengine unaoweza kuwataja kama sehemu ya kikosi cha kwanza cha Chelsea. Lampard anabadilika kila siku.

Ukifanya vizuri ukitokea benchi, basi mechi ijayo unaanza. Uki’flop’ mechi hii, mechi ijayo haupati nafasi. Sijui ukocha lakini, hauwezi kupata muunganiko kwa staili hii.

Kitu pekee ninachoamini ni kuwa, Lampard bado ana nafasi ya kufanya vizuri. Ni kocha mchanga mwenye muda mrefu wa kujifunza.


TENGENEZA FAIDA KUPITIA KASINO YA MERIDIANBET

Neptune’s Richies ni mchezo Unaokupa pesa chap chap huku ukiwa unaburudika kupitia Kasino ya Mtandaoni ndani ya Meridianbet.

Neptune's-Riches_Casino-Post_30-January

Cheza hapa

15 Komentara

    Nikweli kabisa

    Jibu

    Lampard ni kocha ambaye bado anamda wa kujifunza

    Jibu

    Lampard ni kocha mzuri Sana tu na Chelsea watamkumbuka

    Jibu

    Habari njeam

    Jibu

    Lampard alikua na msimu mzuri Sana msimu uliopita

    Jibu

    Habari njema

    Jibu

    Lampard akatafute kambi sehemu nyingine kocha mzuri tu

    Jibu

    Good news

    Jibu

    Wachezaji wa Chelsea wameshindwa kumsoma Lampard

    Jibu

    Kitu kingine anachokikosa Lampard, ni uvumilivu na kutokujua kipi kinamfaa zaidi. Unajua tofauti na ukuta, labda na Mason Mount katikati ya kiwanja, hakuna wachezaji wengine unaoweza kuwataja kama sehemu ya kikosi cha kwanza cha Chelsea. Lampard anabadilika kila siku.

    Jibu

    Chelsea mliwah mno

    Jibu

    Inawezekana pia

    Jibu

    Habari nzuri

    Jibu

    ndo ajifunze

    Jibu

    Lampard alitakiwa kupata muda zaidi wa kujifunza na kufundisha timu kubwa kama Chelsea.

    Jibu

Acha ujumbe