Kocha mkuu wa timu ya taifa ya Spain Luis Enrique amemtetea mchezaji Ansu Fati baada ya kupambana sana kwenye mchezo wa Nations League dhidi ya Switzerland ambapo Hispania iliibuka na ushindi wa 1-0.
Kinda huyo wa miaka 17 ambaye pia ni mchezaji wa timu ya Barcelona na mchezaji mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kufunga katika taifa hilo, alicheza dakika 57 kabla nafasi yake haijachukuliwa na nyota wa Wolves Adama Traore.
Fati alishindwa kutumia vyema nafasi mbili za mwanzo kwenye mchezo huo, na alifanikiwa kupiga shuti moja na hakutengeneza nafasi yoyote ya kufunga kwa wachezaji wenzake.
Lakini pia alishindwa kupiga cross na mfumo wa 3-5-2 wa Switzerland ulidhihirisha kumbana wakati Silvan Wilder na Nico Elvedi walipelekea ugumu kwa upande wa kushoto wa Spain.
“Kukabwa mara nyingi limekuwa ni tatizo kwa Ansu Fati na kila mshambuliaji,” Luis Enrique alisema siku ya Jumatatu ikiwa Spain wanajiandaa kuwakabili Ukraine.
“Malengo yetu ni kutengeneza faida nyingi kwa washambuliaji wetu baada ya hapo kila gemu itakuwa hivyo.
Safu ya ushambuliaji ya Spain pia ilishindwa kufanya maajabu baada ya kwendsa sare ya 0-0 na Portugal wiki iliyopita, lakini safu ya ulinzi ya mabingwa hao wa Kombe la Dunia 2010 inaonekana kuimarika.
Katika michezo 15 ambayo hawajafungwa tangu mwaka 2018, La Roja wameruhusu magoli sita pekee na kuapata clean sheet nane.
Luis Enrique anafurahi kuona wachezaji kama Pau Torres, Eric Garcia na Diego Llorente wakicheza vizuri na anamaamini wachezaji wenye umri mdogo wanaweza wakamsaidia nahodha Sergio Ramos kuimarika.
Naam, hapa ni mahali pako! Kuwa shujaa kwenye sloti hii ya Samurai Ken ujishindie mkwanja na kujipa burudani murua.
Shani
Ansu fat ni kinda ataeibeba Spain kwa muda
Dorophina
Ansu fat ni mchezaji chipukizi anayekuja kwa speed
Povel
Ansu fati anahitaj muda co kpnd hch kumtengenezea zongo juu ya kiwango chake
aisha
Ansu yuko vizuri acha akingiwe kifua maana atafanya mengi sana kwani hata umri wake unaridhisha
Issa
Fat ni mchezaj ambae kiwango chake kitaimarika kadri atakavyopata mechi zaid
Amiri Kayera
Hakua na kiwango kizur
Sabrina
Ansu fundi sina mashaka nae
Flomena
Yuko vizuri sana
Fatuma kasomo
Gud news
Sauda
Kiwango chake hakiridhishi
Elika
Yupo vizur
magdalena
ansu fati ni mpole sana na mkarimu ndo maana ata kocha wake kaamua kumkingia kifua
Angelina
Huyu dogo yuko vizuri
Zeiyana
Wampe mda tu ansu fati ni mchezaji chipukizi hanaye jituma sana
Venerose
Habari njema
Neema
Yuko vzr sana
Tatu
Ansu ni mchezaji mzuri anachotakiwa kwa sasa ni kupewa mda tu
Nasra
Gud news
Mwanahamisi
Yupo vizuri
Ernest
Fati anahitaji muda zaidi
Caroline
Ansu fati anahitaji muda zaidi
Mwajumah
Yupo vizuri
Janeflora malisa
Saf
Saupha mohamed
Good news
Gabriel
Ansu fat ni mchezaji chipukizi anayekuja vizur
Hopemwaikuka
Gud