Nyota wa Barcelona Lionel Messi ni Harry Potter wa kabumbu, hii ni kwa mujibu wa Christian Vieri.
Messi alitoa asisti kwa Ousmane Dembele kwa ufunguzi wa goli la kwanza katika mchezo wa Champions League dhidi ya Juventus na dakika za majeruhi aliweza kufunga goli la pili kwa mkwaju wa penati baada ya kinda Ansu Fati kufanyiwa madhambi eneo la penati.
Mshindi mara sita wa tuzo ya Ballon d’Or alitenegeza nafasi kwa kupiga pasi tano za mwisho na kuisadia Barcelona kujikamatia alama sita na kuongoza katika kundi G.
Vieri, ambaye alishinda Serie A na Juventus mwaka 1996-97 na kuchezea Italy mara 49, amemsifu Messi kwa mchango wake kwenye mchezo wa Jumatano mjini Turin.
“Barcelona yenye maajabu, hakuna gemu ambayo walishinda goli sita saba kirahisi, Walicheza mchezo mzuri,” aliiambia CBS Sports.
“Messi ni mchawi wa soka, ni Harry Potter wa mpira wa miguu na pindi akitundika daruga nitaacha kuangalia soka, sitafanya kazi tena kwenye TV, nitaenda kuangalia Netflix kwa sababu kama akiacha kucheza kutakua hakuna mtu wa kumuangalia.
Ni Christiano Ronaldo pekee katika mashindano ya Champions League ametoa asisti nyingi za magoli (38) kuliko Messi (35) tangu aanze kucheza Champions League mwaka 2004-05.
Tunazungumzia mkwanja wa Tshs.160,000,000! Kupitia Kasino ya Mtandaonii ya Meridianbet unaweza kuwa milionea wakati wowote.
Angelina
Messi hana kazi mbovu
Dorophina
Messi mnyama akiingia uwanjani hatoki hivi hivi barca wangemuachia sijui ingekuwaje
Lydia Emmanuel Magoti
Messi anajua soka kwakweli tuache utani kwamwanasoka huyo hanaitendea kaz yake kwaumakini
Carolyn
Kweli kabisa Messi level nyingineeeee
Khadija
Messi yupo vzr
Mwajumah
Messi yupo vizuri sana
Ester Jackson
Kwa messi na wwchezaji wengine hawako sawa kila mchezaji ananafasi yake na umuhimu wake na ronaldo anajua na messi pia anauwezo wake na hawawezi kufanana viwango kila mmoja ana uwezo wake
Sylvester
Kiukweli ukiangalia Messi anapokua uwanjani huyu jamaa fundi sana,basi aje Uingereza nae akichafue
aisha
Messi hanaga kazi mbovu hasa pale anapoingiaga uanjani hakoseagi
Adelta
Messi Yuko vizuri anajiamini na kazi yake
Sauda
Messi makini sana
Sabrina
Messi mtu mbad
Mwanahamisi
Messi Yuko vizuri
Fatina mfigi
Messi namkubal sana
Elika
Mess yuko vizur sana
Ernest
Messi anaweza akawa msaada mkubwa kwa Barca lakini ikumbukwe pia wachezaji wengine wanatakiwa kujitoa kama Messi katika kupata matokeo, Kadri siku zinavyozidi kwenda tunamuona Messi anachoka sasa ni wakati wa vijanakurithi mikoba japo swala hili linaonekana gumu sana kwasasa ndani ya Barca.
warda
Nilijua tu hii mechi Barca wanshinda
zeiyana
tutasubiri kuona mbadala wa messi kila mchezaji hana viwango vyake kumzidi mwenzie
Hopemwaikuka
Nakubaliana na ww
Issa
La pruga hamn mtu kwenye soka kama huyu
Povel
Ngoj tuone mbadala huo wa la pluga messi e ndapo Kama hataondoka messi nou camp
Saupha mohamed
Mess yupo vuzurii