Milner Aongeza Mwaka Mmoja na Liverpool

James Milner ameongeza mkataba wa mwaka mmoja na klabu ya Liverpool klabu hiyo ya Premier League imethibitisha.

Milner Aongeza Mwaka Mmoja na Liverpool

Mkongwe huyo wa Reds amekubali kupunguzwa kwa mshahara wake ili kuendelea kusalia Anfield inaripotiwa kuzipiga chini ofa kutoka vilabu vya EPL na vile vya ligi ya Marekani Major League Soccer.

Mchezaji huyo ambaye ametimiza miaka 36 aliichezea michezo 61 timu ya taifa ya Ungereza na amecheza mechi 289 Liverpool akiwa amefanikiwa kushinda mataji 6, EPL Champions League, FA Cup, Carabao Cup.

Milner aliiambia tovuti rasmi ya klabu: “Nina furaha sana kubaki kwa msimu mwingine. Sijawahi kuchukulia kawaida kuichezea klabu hii na sitawahi.

“Hisia ya ziada kwangu – na muhimu sana katika mchakato – ilikuwa imani kwamba bado ninaweza kuchangia timu. Mtangazaji alikuwa wazi alichofikiria na hiyo ilikuwa sababu kubwa kwangu kuongeza mkataba wangu.

Alicheza mchezo wake wa kwanza wa Premier mwaka 2002 akiwa na Leeds United lakini pia alivichezea vilabu kama Aston Villa, Newcastle United na Manchester City kwa ujumla amecheza mechi 588 za Premier League.


SHINDA SAMSUNG A32 NA AVIATOR

SHINDA Samsung A32 ukiwa na mchezo wa Aviator kwenye Kasino ya Mtandaoni ya Meridianbet! Kwea pipa ukusanye zawadi zako pamoja na ushindi mnono wa mkwanja!

kasa wa njano, Kasa wa Njano Awapa Ubingwa wa CL Liverpool., Meridianbet

SOMA ZAIDI HAPA

Acha ujumbe