Pep Guardiola ameshawishika kusema kuwa mshambuliaji wa Manchester City Sergio Aguero bado atakuwa “mchezaji yule yule” mara atakaporejea kutoka kwenye matatizo ya majeraha.
Msimu 2019-20, Aguero alipata tatizo la paja na jeraha la goti ambalo lilimfanya kukaa nje kwa miezi minne, akikosa kuanza msimu huu.
Ingawa alirudi uwanjani mnamo Oktoba, Aguero hivi karibuni alikuwa alirudi kwenye chumba cha matibabu baada ya kupata tatizo la msuli wa nyama ya paja, na kwa sasa anauguza jeraha jingine la goti.
Aguero ndiye mfungaji bora wa muda wote wa City na mchango wake katika Ligi ya Premia ni muhimu – tangu msimu 2015-16, amefunga magoli 102 ni Jamie Vardy (106) na Harry Kane (126) ambao wamekuwa wapinzani wake.
Licha ya rekodi yake nzuri mbele ya lango, wengine wana wasiwasi kuwa matatizo ya majeruhi ya Aguero yatasababisha mchezaji huyo wa zamani wa Atletico Madrid kupoteza ukali wake, ingawa Guardiola hana wasiwasi kama huo.
“Atakapokuwa fiti, atakuwa mchezaji yule yule,” Guardiola alisema kabla ya mchezo wa Jumamosi dhidi ya Fulham.
“Kwa kweli, umri ni umri tu, lazima awe sawa na atahitaji muda kidogo zaidi kuliko [Phil] Foden au Raheem [Sterling], kwa sababu mwili wake ni tofauti kabisa, lakini nina matumaini atatusaidia sisi msimu huu kufanya kile anachohitaji.
“Lakini nina imani kwani anafanya kazi sana, ni mtu mzuri, nina uhusiano mzuri na yeye, bora kuliko hapo awali. Ninampenda na tunamtaka arudi haraka iwezekanavyo kwake na kwa timu.”
Aguero yuko mwaka wa mwisho wa mkataba wake huko City, na wengine kwa muda mrefu wanaamini ana mpango wa kurudi Argentina mara tu wakati wake huko Manchester utakapomalizika.
Mchezo wa Astro Legend unakupatia burudani ya muziki kupitia kasino ya mtandaoni ya Meridianbet. Utaburudika huku ukiendelea kutengeza mkwanja mrefu, jiunge sasa na uwe miongoni mwa mabingwa!!
Adelta
Hii ni makala nzuri yenye maelezo mazuri na uhalisi wa wachezaji
Rahma
Shukrani kwa makara
Hopemwaikuka
Mm ni nan nipnge
Mwanahamisi
Asante kwa taarifa
Shakila mrope
Asant kwa makara meridian bert
Khadija
Nice
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri sana
Caroline
Aguero yupo juu
Issa
Kun aguero majeraha yamemfany awe nje ya kiwango
Magdalena
Aguero no MTU wa tofauti
lombo
saf
Neema
Na aminii hawezi badilikaa
Dorophina
Aguero yupo vizuri sana
Latifa juma mohamed
Habari njema.
Saupha mohamed
Safi
samiah
Safi
neema hassan
Habari njema kwa mashabk
felister
ahsante kwa taarifa
Tatu
Kijana yupo vizuri
Sabrina
Aguero fundi huyo
Janeflora malisa
Saf
Sauda
Aguero jembe
Tahiya
Vizur
[email protected]
Vzr sana
aisha
Duuh kazi anayo tatizo majeraha ndio shida
warda
Anaweza baki yule yule anaweza badirika sema Pep anajipa matumain tu