Mshambuliaji Lionel Messi anayetaka kuondoka kunako klabu ya Barcelona “atacheza popote anapotaka” na yupo vizuri kuwa mchezaji bora katika ligi atakayo kwenda, hii ni kwa mujibu wa Mauricio Pochettino.
Messi ameitaarifu Barca hamu yake ya kutaka kuondoka klabuni wiki iliyopita na inaarifiwa kwamba anaweza akaondoka kwa uhamisho huru baada ya kupitia vifungu katika mkataba wake ambavyo vinamruhusu kuvunja mkataba.
Lakini, Barca na LaLiga wanataka malipo yafanyike kama Messi akitaka kuvunja mkataba na dau la €700m litatakiwa kulipwa ili aruhusiwe kuondoka katika klabu hiyo ya LaLiga.
Baba wa nyota huyo wa Argentina ambaye ni wakala wake bwana Jorge Messi amekutana na rais wa klabu ya Barcelona Josep Maria Bartomeu siku ya Jumatano kwaajili ya mazungumzo kuhusu Messi kuondoka na kuhamia Manchester City klabu iliyoonesha nia ya kumsajili Messi.
Na Pochettino, ambaye kipindi cha nyuma aliwahi kuhusishwa kuchukua nafasi ya Setien kabla ya Koeman haja lamba dili ya kuinoa timu hiyo, anatarajia mtaifa mwenzake huyo aseme neno la mwisho kuhusu hatma yake.
“Lolote linaweza likatokea, Messi anaweza kucheza popote anapotaka ndani ya Spain au Premier League. Yupo tayari kuwa mchezaji bora ligi yoyote,” Pochettino aliiambia Argentine outlet Ole.
Pochettino amekuwa bila timu tangu aondoke Tottenham mwezi Novemba na alikuwa akitizamiwa kutua Camp Nou kufuatia kuondoka kwa Quique Setien mwezi uliyopita.
Mchezaji huyo wa zamani wa Espanyol na kocha wa miaka ya hivi karibuni aliwahi kunukuliwa akisema kwamba “ni bora afanye shughuli za kilimo kuliko kuifundisha Barca.
Siku za hivi karibuni alirudi tena kwenye media na kusema “anajutia usemi wake na hakuwa sahihi kutamka vile sababu huwezi jua nini kitatokea katika maisha.
SHINDA NA HI LO
Sasa hii ni rahisi zaidi kupata USHINDI! Unatabiri karata ipi ipo chini au juu, kisha unakusanya mkwanja wako.
Furahav
Huyu messi nae siaende anapotaka kwenda tuuu.
Dorophina
Kazi sasa kwa vilabu kutafuta hilo day la kumfanya Messi kuondoka Barca man city nafasi ndio hii wajitutumue
magdalena
messi aende tu kokote kambi
Shani
Haya maneno sasa
Ernest
Barca wanatakiwa kuheshimu uamuzi wa Messi kama heshima amewatengenezea heshima kubwa sana kwenye ulimwengu wa soka, now its time for them to be fair enough and see how they will overcome the situation.
Nasra
Messi yuko vzuri popote
Povel
Shida co kucheza ishu ni kupaformu timu akayokwenda kucheza na heshimah watakayo mpa je itafikaha kama ya nou camp au argentina ngoj tuone movie hiii itakwisha je
Caroline
Kweli kabisa wasimpangie
Sauda
Mwacheni aende anapoona panamfaa.
Mwajumah
Messi nenda popote tu unapotaka kwan kambi popote#Meridianbettz
Fatina mfigi
Messi nae anatuchangany kokote kambi si aende anapotaka yy!!
rama
itakuwa vizuri sana messi wamuache tu aondoke barcelona akalete ushindani ligi nyingine
Frank P
Maisha yanaenda kasi sana
Mwanahamisi
Messi namkubali sana
Saupha mohamed
Messi unakwama wapi kokote kambi mzee
Tatu
Maamuzi ni yake popote anaweza kwenda kucheza
Lydia Emmanuel Magoti
Nikweli kabisa Pochettino anacho kisema Messi atacheza anapo pataka yeye uwamuzi niwake yeye Kama yeye Messi
felister
aya ndo mambo niliyokua nataka kuyasikia
aisha
Safi sana messi nimeipenda mnoo
Neema
Maamuzi ni yake mwenyewe
Amiri Kayera
Kwa umri wake naona anatafuta pa kumalizia mpila wake tu
Theonestina
Sawa afanye tu anavyotaka
Rehema
Ni maamuzi yake mwenyewe
Rose kapinga
Afanye chaguo mwenyewe,wapi panamfaa kuendeleza kandanda!!
Sabrina
Messi jeshii yuko vizur
Genia Sikaluzwe
Messi ni mchezaji mzuri popote anacheza
kabogoro
Maoni: kiukweli kwa uwezo wa messi anaweza kucheza timu yoyote ile hata akija yanga freshi tu.
Theckla
Yuko sahihi
Shafii
Yuko sahihi sidhani Kama kuna timu duniani kote itakua haimuhitaji messi la! hasha.
Ester jackson
Barcelona inaonekana kuwa bado wanataka mana sio kwa sheria hiyo ambayo wameweka ya kuvunja mkataba kwa hela hiyo mana wanajua kuwa uchumi umeshuka sana na isitoshe lion messi ni mchezaji ambaye anajua anacho kifanya .ndiyo mana wameweka hivyo ili kumkomoa tu wamuache tu aondoke kuliko kumpotezea mda tu
farida ahmadi
Yuko sahihi kabisah asemavyo kocha wa Spurs
Zeiyana
Ni kweli messi hana uwezo was kwenda kuchezea maali popote ila kwa mahamuzi yake ya sasa sio sahihi kwa clabu ya Barcelona ukiangalia kabic bado wanaumimu nae
Adelta
Messi maamuzi Ni yake mwenyewe
@meridianbettz
Samiah
Uwamuzi niwake
Issa
Mess kuondoka barca ni swala gumu kwa kuwa barca haitawwz kumruhus kirahis itabid timu inayomsajil imwage mpunga mrefu
Sadick
Messi ni kama dhahabu jinsi ilivyopendwa na kila mtu#meridianbettz
Hope mwaikuka
Hebu mpumzshen kdogo afanye anachotaka bas
Gabriel
Messi kama heshima amewatengenezea heshima kubwa sana kwenye ulimwengu wa soka
Tahiya
Kwer afanye maamuz yake hasichanganywe watu
warda
Messi Mwoga sana Hawezi toka Barca