Zinedine Zidane amesema kwamba hatokaa Real Madrid kwa kipindi kirefu na anatarajia kustaafu mapema kuliko vile inavyo dhaniwa.
Zidane amekua na matokeo chanya hapo Los Blancos, kwa miaka mitano aliyo itumia akiwa kama mchezaji na sasa akihudumu kama kocha.
Wakati alipo anza kuinoa Madrid kwa mara ya kwanza aliipatia mafanikio ya kihistoria kwa kuweza kunyakua taji la klabu bingwa Ulaya mara tatu mfululizo, ingawa aliondoka mapema,mara baada ya kushinda taji la tatu, alirudi tena mwaka uliyopita kufuatia Madrid kutofanya vizuri chini ya Satiago Solari.
Amerudi Los Blancos akiwa na moto kwa mara nyingine akiwa analiwinda taji la La liga wakichuana vikali na Mahasimu wao kutoka Katalunya Fc Barcelona wakiwa wanafanana pointi lakini Madrid wapo nafasi ya kwanza kwa faida ya kushinda mechi walizokutana.
Lakini ni nadra kwa Zidane kufanya ukocha kwa kipindi kirefu, kwani hata kipindi alipokuwa hajishughulishi na kazi hiyo alikuwa akifanya kazi nyingine tu nchini kwake Ufaransa.
Ikiwa anaelekea kukutana na timu ya iliyo nafasi ya mwisho katika msimamo Espanyol, ambayo imemfukuza kocha wake Abelardo mapema,Zidane alizungumzia malengo yake ya baadaye pia aliulizwa kuhusu Ramos.
Alipo ulizwa kama Ramos anaweza kuweka alama katika klabu akiwa anacheza kama beki wa kati, alijibu anaweza kufanikisha, sababu ana kiwango kizuri akiwa kama mchezaji na maisha yake kwa ujumla.
“Mara zote amekuwa akitaka ushindi na kuweka historia katika klabu,si shangazwi na akifanyacho, ni bahati kuwa naye katika klabu ya Madrid nadhani ataendelea kufanya hivyo mpaka atakapo staafu. Siendi kufundisha kwa miaka 20 nitastaafu muda si mrefu, chochote kinaweza kutokea.”
Aliongeza: “Nilikuwa mchezaji mzuri sana kuliko ukocha, lakini kulikuwa na wachezaji wazuri zaidi yang, ingawa nina furahia kwa nilicho kifanya kwenye soka.”
“Sitafundisha kwa kipindi cha miaka 20,sijui kwa muda gani, sijapanga chochote nafikiria kufanya mambo mengine.
Neema juma
Sio mbaya kwa kwa uamuzi alioufikiria yeye
Amiri Kayera
Safi lazma aweke na mda wakupunzk sio mpila t kila ck
Hidaya
Kazi na umri pumzika tu upishe kipaji kingine
Hamidu
Asante kwa taarifa#meridianbettz
Gabriel
Zidane bado nikijana kabisa kwny orodha y makocha hivyo asionyeshe kuchoka mapema kwan kuitumikia club kubwa Kama hiyo n fahar sana kwake
# meridianbet Tanzania
neema hassan
Asante kwa makala
isha
Mzee amechafuka sawa baba tumekuelewa kila la kheri huko uendako kapumzike salama baba
Furahav
Uko sahii,mana kufundisha mpira sio kazi raisi.
farida ahmadi
Zidane ni kocha mzuri Sana pia amefundisha Madrid kwa muda mrefu Sana na ameiendesha klabu ya Real Madrid vizuri na kutwaa ubingwa mara nyingi sio mbaya akipumzika kufundisha timu ya Madrid kutokana na umri pia umeenda inabidi hastaafu tyuu
warda
Zidane mjanja Anataka kustaafu kwa Heshima #Meridianbettz
Ester jackson
Zidane kocha bora anetumia akili nyingi na kuwafanya bahadhi ya wachezaji wamepata mafanikio kupitia yeye na kuweka historian katika timu hivyo bado anauwezo wa kuendelea kuwa kocha bado real Madrid wanamuhitaji ingawaaamuzi bado ni yake kubaki au kuondoka
Njiku
Zidane ni kocha mchanga sana na kuifundisha timu kama real madrid ni bahati sana kwa heshima ya klabu imempa nafasi hyo kama regindali wa zamani wa timu kocha mdogo timu kubwa
Theckla
Maamuzi mazuri
Samiah
Makala nzuri sanaaa
Povel
Thnks meridian bet tz kwa update za michezo na burudani
Edgar
daah kwanini tena zidane madrid itapwaya bhna
Tahiya
Zidane mbona kama unatutenga ivi
Hope mwaikuka
Ni uamuz wake mm nitapngaje
Omary lukumbi
Kwanza zidane mjanja sana anataka kustaafu bila kualibu rekodi yake ya kufundisha mpira anataka kuondoka kabla mambo hayaja halibika
mwakalosi
mzee anapima upepo tu
David Pere
Kazi yake ni kufundisha soka ,ni kweli hawezi kuka pale kwa muda mrefu sababu anaweza akatakiwa na timu nyingine akawnda kufundisha
Salma
Uwenda plan zake hataki kuzeekea hapo
Ester mmakasa
Jamani zidane bado yuko vizuri apige kazi.
Evaluziga
Ametumia maamuzi mazuri
Latifa juma mohamed
Uamuz sio mbaya
fatumakasom
Safi tu uamuzi ni wake
Theonestina
Kweli kabisa.afanye maamuzi tu
Elika
Safi sana inabidi astaagu tuu awaachie na wengine
JULIANA
Jamani Zidane mbona uko vema kwenye ufundishaji mpira
Dorophina
Sio mabaya maamuzi yake zidane ameitoa timu ya madrid mbali sana Ni mda wa kustaafu sasa
felister
Zidane usituache ivy jamani real bado tuna kuhitaji
Zeiyana
Zidane bado kijana hivyo asioneshe kuchoka mapema pia kufundisha clabu kama madrid ni bahati kubwa sana
lombo
safi habar njema
Caroline
Zinedine zidane ameshachoka
nasra
Uamuzi mzuri
Genia Sikaluzwe
Zinedine zidane hata hivyo umli umenda kwa sasa uwamzi wake mzuri
Sadick
Sikufurahia kabisa alipostaafu soka mapema , anatakiwa kuendelea kutoa mchango wake katika Ulimwengu wa Soka#meridianbettz
Angelina
Angebaki ili alete chachu kwwnye soka kustaafu mapema haijakaa sawa
Mariam mtandama
Makala mazur
Isaya massawe
Hakuna chenye mwanzo kisichokua na mwisho
Sabrina
Maoni:Zinadine mbona anastaafu mapema alafu soka bado linamuhitaji inabidi afikilie huu uwamuzi wake.
Shafii
Kiukweli kazi ya ukocha ni ngumu Sana kocha anapopata mafanikio makubwa katika clubu anastahili pongezi Sana maana anafanya kazi ambayo ni vigumu Sana kupumzisha kichwa
tumaini
Maoni:makala nzuri sana
Adelta
Yuko sahihi kwa maana kufundisha mpira sio kazi rahisi
Magdalena
Maamuzi yake hatuwezi kuyapinga Kama kashaamua kusepa sawa achape lapa
Christa
Ni vema kistaafu mapema ukiwa bado akili haijachoka
Fatina mfingi
Ni bora lakin