Diego Simeone amevutiwa na kasi aliyoanza nayo Luis Suarez na amevutiwa zaidi na asisti aliyotoa kuliko goli mbili alizofunga kwenye ushindi wa 6-1 dhidi ya Granada siku ya Jumapili.
Suarez aliingia kipindi cha pili dakika ya 70 ya mchezo na ndio ulikuwa mchezo wake wa kwanza tangu ajiunge na Atletico Madrid na aliweka wavuni goli mbili na kumtengenezea asisti mchezaji mwenzake Marcos Llorente.
Mchezaji huyo ambaye ni mtaifa wa Uruguay alijiunga na klabu ya Atletico Madrid kwa dau la €6m akitokea klabu ya Barcelona, katika mchezo wa jana alifanikiwa kutengeneza penati ambayo VAR iliikataa.
Suarez alifunga magoli mawili, moja alifunga kwa kichwa na lingine alifunga baada ya kupiga shuti lililogonga mwamba na kukutana nao tena kisha akamalizia lakini kocha mkuu wa Atletico amekiri kuipenda zaidi asisti aliyompa Llorente aliyetokea benchi.
“Magoli yake mawili ni ya kawaida kwangu mimi lakini ile asisti ni nzuri sana,” Simeone alisema baada ya kumalizika kwa mechi hiyo.
Diego Costa, Joao Felix na Angel Correa walifunga katika mchezo huo uliyo malizika kwa Atletico kuibuka na ushindi mnono wa 6-1 katika dimba la Wanda Metropolitano na kuweka rekodi ya kushinda kwa goli nyingi katika mchezo wa ufunguzi wakiwa chini ya Diego Simeone.
Atletico watawabana mahasimu wao Real Madrid na Barcelona msimu huu na Simeone anaimani ushindani utakuwa mkubwa baada kila timu kujiandaa vizuri.
“Itategemea kutokana na kazi yetu, Ujio wa Suarez umeongeza chachu ndani ya kikosi chetu na kama wachezaji wote 23 watazithamini dakika za kucheza hakika tutashinda vizuri.
Beti kwa Kitochi Kushinda 300,000,000!
Unajua kuwa unaweza kushinda milioni mia tatu kwa buku tu? Ndiyo! Unaweza kushinda kwa kupiga *149*10# na kubashiri. Ingia mchezoni!
lombo
habar njema
magdalena
suarez yupo makini sana
Dorophina
Suarez mwamba
Gabriel
Deal done 👍
Mwajumah
Habari njema
Adelta
Suarez Yuko vizuri
Tatu
Safi sana kijana mwazo mzuri
Lydia Emmanuel Magoti
Namkubali Sana Suarez mzee wakutikisa nyavu akoseagi
Samira
Siku zote Suarez ni bora sema barcelona hawakutaka kumpa mda
jullie
hongera zaKE
Amiri Kayera
Suarez atafanya mengi San pale A.madrid
aisha
Suarez anajua wajibu wake kwenye soka
Povel
Suarez ni mmoja ya mafowadi hatari Sana duniani
Theonestina
Safi
Issa
Huy ndio suarez ukizubaa anakuweka tu hana maaihara nyavuni
Khadija
Habari njema
Hopemwaikuka
Kama cjaelewa
Sabrina
Suarez yuko vizuri sana
Ester jackson
Mwanzo mzuri sana hapo ndio Barcelona watajua umuhimu wako
Rehema
Safi
Theckla
Ameanza vizuri
Saupha mohamed
Jambo zuri
Genia Sikaluzwe
Jambo jema
Shani
Suarez ni makin sana
Tumaini kasalile
Yuko poa
Sauda
Suarez yupo vizuri sana
Samiah
Suarez mtu mmbaya
Venerose
Safi sana
farida ahmadi
Safiiii Sana
Mwanahamisi
Jambo zuri
Nasra
Yuko vzuri
Zeiyana
Suarez hanazidi kuonesha mahajabu yake na ndio maana Barcelona waliamua kumuuza mbali na wapinzani wao wanaijua shuuli yko
Janeflora malisa
Good
Ester mmakasa
Safi sana Suarez .
Angelina
Suarez yuko vizuri
Rose kapinga
Safiii hiyoo
felister
deal done
Fatina mfigi
Safii
Latifa juma mohamed
Namkubali Sana.
Ernest
Mwanzo mzuri kwa Suarez
David Pere
Huy ndio suarez ukizubaa anakuweka tu hana maaihara nyavuni