Mshambuliaj Wolves, Raul Jimenez, 28, amesema itakuwa ngumu kukataa ofa kutoka kwenye vilabu vya Hispania Real Madrid and Barcelona.
Golikipa wa Manchester United, Dean Henderson, 23, ambaye ametumikia kwa mkopo msimu 2019.20 akiwa Sheffield United, anatarajia kuendelea kutumia mwaka mwingine nje ya klabu.
Straika wa Lyon, Moussa Dembele, 23, amehusishwa kuwindwa na Manchester United lakini klabu hizi mbili hazijafanya mazungumzo.
Kiungo wa Chelsea, Willian, 31, amesema haina tatizo kuhamia kwenye klabu hasimu jijini London – lakini hakujata aidha ni Tottenham au Arsenal.
Winga wa Bournemouth Ryan Fraser, 26, amewaambia marafiki zake anatamani kujiunga na Tottenham kipindi hiki cha kiangazi kama watamhitaji.
Kiungo Atletico Madrid Hector Herrera, 30, ni mmoja ya wachezaji waliowindwa na West Ham katika dirisha la usajili Januari na wakashindwa kunasa saini yake, lakini bado wanajaribu kumsaini kipindi hiki cha kiangazi.
Winga wa Valencia Ferran Torres, 20, amemshauri mchezaji mwenzake Jose Luis Gaya, 24, asikubali kusajiliwa na Liverpool.
Mshambuliaji wa Barcelona, Philippe Coutinho, 27, yuko nje ya bajeti ya Leicester City, amesema kocha Brendan Rodgers, pamoja na uvumi kipindi hiki cha kiangazi.
Mchezaji mpya wa Watford Pape Gueye, 21, hataki tena kucheza Premier League pamoja na kusaini mkataba wa miaka mitano kwasababu anahofia atatolewa kwa mkopo.
Liverpool wamewasiliana na beki wa Napoli Kalidou Koulibaly, 28, kama mbadala muhimu wa Joel Matip.
Tottenham wameanza mazungumzo ya kusaini beki wa Hellas Verona, Marash Kumbulla, 20, kama mbadala wa Jan Vertonghen.
Frank Patrick
Hawa Liverpool hawa
Zainabu
Huwezi kataa ofa ya vilabu vikubwa kama bacelona
Mathayo sonje
Naona in vizuri inapotokea ofa kama hizi kwa wachezaji inakua ni fursa kwao
Ernest Kimeru
Muda wake sasa kwenda kukipiga kwenye timu kubwa zaidi!!!
furahav
Changamkia fursa hiyo Raul.
JULIANA
Masilai kwanza
Mwanaidi
anatakiwa achangamkie fursa ila kikubwa aangalie na maslai yake
Samira
Fursa ya kutembea nayo
Povel liwongolo
Muda umefika kwenda kutafuta changamoto sehemu nyngne
Amani
Raul nibora akaenda kweny timu zinazo muitaji
Tahiya
Ni ndoto kwa kila mchezaji kuchezea timu kubwa ili kujitangaza zaid
Gabriel
Big deal
Mwanahamisi
Atizame masilai Kwanza
Lydia Emmanuel magoti
Achangamkie fulsa yake ndokinachotakiwa
Shafii
Hakuna mchezaji atakaye pinga kwenda timu kubwa
Fatina
Safi
isha
achangamkie tuu fulsa
farida ahmadi
Kambi popote