Mashabiki wa Sevilla na Bayern Munich wataruhusiwa kuhudhuria mechi ya UEFA Super Cup mwezi Septemba 24 katika dimba la Puskas Arena.
UEFA imethibitisha mashabiki wataruhusiwa kuwepo uwanjani, Budapest kwa mchezo utakao wakutanisha Mshindi wa Champions League na mshindi wa Europa League lakini kutakuwa hakuna zaidi asilimia 30 ya siti zitakazo ongezwa.
Maamuzi tayari yamefanywa kwa hiyo baraza linaloongoza limeangalia kama kutakuwa na athari kwa mashabiki pindi mchezo huo utakapo chezwa hali ya kuwa bado kuna janga la virusi vya Corona.
Puskas Arena
Rais wa UEFA aleksander Ceferin amesema: “Wakati kumekuwa na umuhimu kuonesha kwamba mpira wa miguu unaweza kendelea hata kwenye nyakati ngumu, kucheza bila mashabiki, mchezo umepoteza ladha yake.
“Tunafanya kazi kwa ukaribu na chama cha mpira cha Hungari na Serikali yake katika kuhakikisha usalama wa kiafya kwa watu wote watakao hudhuria katika mchezo huo.
“Hatuto hatarisha usalama wa watu .”
Bayern wamefuzu kuwania kombe hilo baada ya kuibuka mabingwa wapya wa Champions League kwa kuwafunga PSG 1-0, wakati Sevilla walifanikiwa kufika hatua hiyo kwa kuwafunga Inter Milan 3-2 katika fainali ya Europa League.
Tovuti ya UEFA imetaja uwanja wenye uwezo wa kubeba watu 68,000 utaruhusiwa kubeba watu 20,000 katika mchezo huo wa UEFA Super Cup.
Beti Mbio za Mbwa Mubashara
Hii ni rahisi zaidi! Hapa USHINDI unaupata kwa kuchagua mbwa anayeshinda mbio na machaguo mengine yenye odds tamu.
Asia Abdy
Hyo ni habar njema sana
Dorophina
Habari njema hii dhaa shangwe zinaanza kurejea budapest
Ester jackson
Hii itakuwa powa sana kwa mashabiki
rama
habari njema sana kwa mashabiki wa mpira
Tatu
Habari nzuri kwa mashabiki wa kandanda
felister
habari njema kwa mashabiki wa mpira wa miguu
Neema
Habari njema hii
farida ahmadi
Habari nzuri Sana
Latifa juma mohamed
Wakati kumekuwa na umuhimu kuonesha kwamba mpira wa miguu unaweza kendelea hata kwenye nyakati ngumu, kucheza bila mashabiki, mchezo umepoteza ladha yake lakini kwa taarifa ya leo tumefurahishwa mashabiki nasi tukiwa uwanjani kushuhudia.
Gabriel
Imekaa poa sana 👍
Sabrina
Inapendeza
Lydia Emmanuel Magoti
Safii imependeza sana
Furahav
Safi
magdalena
mambo mazuri tuliokuwa tunayasubiri yaja
warda
Afadhali bwana