Barcelona walikuwa wanaongoza mbili kwa moja dhidi ya Chelsea. Hapo John Terry ametolewa nje mapema sana. Kumbuka mechi ya kwanza darajani Chelsea walishinda kwa bao pekee la Didier Drogba. Kama ingeisha hivi, Chelsea walikuwa wanakwenda fainali ya UEFA.
Lakini ilionekana kama ‘HAIWEZEKANI’ kwa Chelsea. Utawadhibiti vipi Barcelona kwa dakika 45 wasikufunge mkiwa pungufu??
Nikiwa katikati ya mashabiki wachache wa Chelsea, jamaa mmoja aliniambia, “Acha mashaka, Chelsea inakwenda fainali” Kusema ukweli, SIKUAMINI.
Si kwamba naishabikia Chelsea. Si kwamba nili-bet kwa Chelsea, bali nilitaka Chelsea watwae UEFA kwasababu ya mwanaume mmoja wa kiafrika, ‘DIDIER DROGBA’.
Kwa miaka mingi niliishi nikimhusudu sana askari huyu. Niliishi nikihusudu mapambano yake na nilitamani sana afanikiwe kutwaa ndoo ya Ulaya.
Dakika ya themanini, Mwili wangu ukiwa unatetemeka kwa baridi, mkononi nimeshika tochi na mwamvuli wangu. Nazifikiria kilometa za kukanyaga kurudi nyumbani, tena mvua ikiwa inanyesha.
Roberto Di Matteo alimnyanyua Fernando Torres. Saa hiyo Chelsea wapo ndani ya box lao wote, wawazuia watoto wa Catalunya. Kumbuka Barcelona wanahitaji bao moja tu wasonge mbele.
Kila mtu akiwa anazifikiria dakika za muda uliopotea, Didier Drogba ameshindwa kukaa kwenye kiti, amezuiliwa ili asiingie uwanjani.
Saa hiyo mashabiki wa Chelsea wamenywea! Si waliokuwa Camp Nou wala waliokuwa ndani ya vibanda umiza nyumbani Tanzania waliokuwa na nguvu ya kuzungumza.
Barcelona walipiga shambulizi, Chelsea walizuia na mpira ulioshwa mbele. Fernando Torres alikuwa mwenyewe katikati, kwasababu Barcelona walipanda mbele wote. Torres alikimbia na mpira kisha akamfuta golkipa Victor Valdes na kuweka mpira kambani.
Chelsea wakatinga fainali ya Ulaya na Didier Drogba alikwenda kutwaa ndoo ya Ulaya.
KWANI MERIDIANBET WANASEMAJE! MKWANJA UPO KWENYE KASINO MPYA YA MINI POWER ROULETTE.
Unawezaje kukosa ubingwa ndani ya kasino hii maridhawa, Nafasi ya kushinda mkwanja ni kwa kila mtu, Meridianbet inakupa nafasi ya kuwa mmoja ya washidi leo, unasubiri nini?
Issa
Torres alikua matata san
Chiku
Torres kawatolea watu uvivu
Magdalena
Ilikuwa ni balaa sana
Adelta
Torres wako vizuri
Sarah
Hatari sana
neema hassan
Duuh
Adelta
Torres wako vizuri
Caroline
Torres noma
aisha
Duuh jamaa noma sana
dorophina
Torres yupo vizuri sana
sauda
Noma sana
Sania mapua
Torres noma
Lydia Emmanuel Magoti
Torres yupo vizuri