Ujerumani watampa Lionel Messi pasipoti ya kusafiria kama atajihisi kutokukubalika na taifa lake, aliongea katika hali ya utani Lothar Matthaus, ambaye angependa kuona Messi akicheza katika ligi ya Bundesliga.
Messi ameshinda mataji 34 akiwa na Barca, lakini ameshindwa kuyafikia mafanikio hayo katika timu ya taifa kwa kupoteza fainali nne kubwa akiwa ana timu ya Taifa bado anapambana kuleta kombe kwa timu ya taifa iliyo shinda tangu mwaka 1993.
Ukweli ni kwamba muda mwingi Messi ametumia maisha yake kuwa Spania, na mara nyingi amekuwa akikosolewa na Argentina kwa kushindwa kuipatia mataji ya kimataifa kama vile Kombe la dunia na Coppa America.
Messi amekuwa akifananishwa na mtaifa mwenzake Diego Maradona, ambaye hakupata mafanikio mengi katika ngazi ya klabu lakini alipelekea Argentina kushinda kombe la Dunia mwaka 1986.
Matthaus ameongelea kuwa jinsi Messi anavyo chukuliwa na taifa lake ametoa maoni kuwa Ujerumani ipo tayari kumpa Uraia.
“Siwezi kuamini hii, kama humtaki Messi anaweza kuja Ujerumani muda wowote, tunasubiri jambo hilo litokee tutampa Pasipoti. Nashindwa kuwaelewa ,” aliiambia Nacion Matthaus ambaye alishinda kombe la Dunia na Ballon d’Or mwaka 1990.
“Mazungumzo ni yale yale kati ya Messi au Maradona yupi ni bora . Argentina wana bahati kupata wachezaji hawa wawili wakubwa, na wanabishana yupi ni bora kati yao? Tafadhali.“Wanawachezaji wawili pekee wakubwa katika historia ya mpira nchini mwao.”
Imekuwa ikiripotiwa kuna kipengele kitacho mruhusu Messi kuondoka Barca kwa uhamisho huru akimaliza msimu.
Messi mwenye umri wa miaka 33 anatarajia kuongeza mkataba hapo Camp Nou, lakini Matthaus amgependa kumuona mtaalamu huyo akisakata kabumbu katika ligi ya Bundesliga
“Kwakweli tungemchukua, tungefurahia kama tungepata nafasi ya kuwa na Leo katika ligi ya Bundesliga,” alisema Matthaus.
“Lakini nakubaliana nao: Nina furaha kuwa na mtu kama Messi kwenye kandanda.Ni mchezaji mkubwa na ni mtu mzuri sana.
“Namfahamu Messi binafsi na ananifurahisha na mtindo wake wa uchezaji.”
lombo
mess bila Barcelona hawez kufanya lolote
Magdalena
Kujikwaa ukaanguka hakumaanishi safari ndo imeishia apo ata Messi atajiangalia wapi alikosea ili ajisahahihishe afikie malengo
Njiku
Matthau’s yupo sawa kwa kuwa Messi ni mchezaji mzuri sana kama muandishi anavyosema kuwa anamataji 34 aliyopata kwenye timu yake ya klabu ya barcellona,Messi alitaka kustaafu kuichezea timu yake ya taifa ya Argentina Ila raia wa Argentina hawakutaka kumuona Messi kuacha kucheza katika timu yao ya taifa licha ya kufanya vibaya katika timu yake ya taifa mashabiki bado wanampenda sana,MATTHAUS alitamani Messi anyone Ujerumani hahaha kitu ambacho hakiwezekani
Leonard
Messi atabaki kuwa muagentina tu
Hamidu
Messi Barcelona ndo nyumba kwao! Huyo atamalizia soka lake hapo caturunya.#meridianbettz
Genia Sikaluzwe
Mess ni lazma aendelee kubaki Barcelona agentina ni nyumani
Lydia Emmanuel Magoti
Messi bila Barcelona awezi kufanya lolote Barcelona ndio mama kwampambanaji huyo
Issa
Mess ni mzuri sema anatakiwa aende kwenye ligi nyingine akutane na challenge
Mpya aonyeshe ubora wake
Furahav
Messi ni mchezaji nzuri kwenye klabu sio timu ya Taifa.
isha
Duuh hatari sana kumbe barcelona ndio imemuinua messi basi kumbe arudi barcelona ili akaendelee kufanya maajabu
felister
Messi inabidi atoke Barca aende klabu nyengine ili apate changamoto nyengine
Hope mwaikuka
Messi popote anafit tu
Ester jackson
Yuko sahihi matthaus kwake anatamani messi aende ujeruman lakini pia akumbuke kuwa messi hawezi kwenda mechi nyingine zaid ya Barcelona ingawa alishawishiwa na kikosi hicho kusaini mkataba wa kudumu na kuukataa inavyoonekana messi anataka acheze hapo Barcelona mpaka atakapo staafa ingawa utani unaleta chachu ya Mabadiliko
Dorophina
Barelona wanamtegemea sana messi
Caroline
Messi na Barcelona ndo panamfaa
Devotha
Messi na Barcelona, Barcelona na Messi
Ernest
Vituko hivi
Frank Patrick
Anachangamoto moja tu hispania bhas mnatarajia aisaidie team ya taifa kubeba ndoo?
Saupha mohamed
Messi mchezaji wakimatifa …akii tu n Barcelona
Gabriel
Japo tunaweza kusema utani lakini Matthau’s alichokiongea yuko sahihi sana kwa staa huyo maana kuna kipindi kulikuwa kunaskendo nyingi sana kumuhusu messie na baba yake kutolipa kod na baadhi ya skendo kibao ambazo linamfanya star huyu kushushwa hadhi yake kwa kitendo cha kuongea hicho alimaanisha kabisa
Maana star Kama huyu alipaswa kupewa heshima kubwa sana katika taifa lake Kama mastaa wengine Kama Zidane ambaye alitengenezewa had Sanam ,mwingine Neymar ,CR 7 na wengine wengi tunaona mataifa yao wakipewa heshima kubwa sana hivyo natambua Kama kwel messie angepata uraia wa ujeruman na kwa uwezo wake basi ata sanamu ya Messi ingetengenezwa huko ujeruman
Kwa upande wangu naamin Matthau’s alikuwa anaongelea utani kwa kumaanisha Jambo la kwel
Hv nice update 👍
# meridianbet Tanzania
Khadija
Messi na barcelon ndio panamfaa#meridianbettz
Mwanaidi
Messi inabidi aende klabu nyengine abadili upepo kidogo
Sadick
Kila mpenzi wa mpira atakwambia Messi ana vitu adimu kwa wachezaji wa siku hizi ni bahati mbaya hajapata mafanikio katika timu yake ya Taifa#meridianbettz
Agness
Messi na Barcelona damdam
warda
Kinachomshinda Messi kupeleka ubigwa kwao Wenzake hawana bidii sana#Meridianbettz
Sabrina
Maoni:mwenyewe inaonyesha mapenzi yake yapo Argentina.
Omary lukumbi
Anaweza tuu kufanya hvyo maana inaonesha timu yake ya taifa argentina kama diego costa tuu kwenda spain
Shafii
Messi popote pale anapawasha kwani mwanajeshi hachagui uwanja wa vita messi jembe Sana
David Pere
Ukiangalia Sana Kama kweli ni utani lakini ni kweli kabisa
Samiah
Popote kambi kwani Messi ni fundi ambae haogopi chochote
Evaluziga
Mess na Barcelona damdam
Elika
Mess ni wa Barcelona tuu hakuna cha zaidi
Zeiyana
Star kama messi alipaswa kupewa heshima kubwa sana katika taifa lake kama mastaa wengine wakina neymar,cr7,zidane na wengine wengi tunavyo on a mataifa yai wakiwapa heshima..!matthau’s alikua hanaongea utani wa kumaanisha na ukweli
Povel
Gud news
Angelina
Utani unaweza kuwa kweli
Amiri Kayera
Mess aitaji changamoto me naon akitok Barca analud kwao Argentina
Salma
Abaki hapo hapo ana miaka mingi ya kuzeeka
Emmy cleopa
Ahsante kwa taarifa
Tatu
Abadili upepo kila siku Barcelona na Argentina timu nyingine zinamuitaji ingawa itakuwa ni vigumu kwa Barcelona kumuondoa mess