Borussia Dortmund wanaripotiwa kuwa wapo tayari kumuuza Jadon Sancho kwa pauni milioni 88 wakati wa dirisha la usajili la majira ya kiangazi.
Mchezaji huyo wa miaka 20 alihusishwa sana na kuhamia Manchester United mwaka jana, lakini BVB walidaiwa hawakuwa tayari kushuka bei ya pauni milioni 108 kumuuza mchezaji huyo wa kimataifa wa Uingereza.
Sancho amepata changamoto katika kuonesha ubora wake katiika kiwango ambacho alitarajiwa kwa Dortmund kipindi hiki lakini bado ameweza kuchangia mabao nane na kutoa asisti 13 katika mechi 25 kwenye mashindano yote.
Ripoti ya hivi karibuni ilidai kwamba kuwasili kwa Amad Diallo huko Old Trafford kunaweza kuwafanya Mashetani Wekundu kusitisha harakati zao za kumnasa Sancho, ambaye bado ana mkataba hadi 2023.
Hata hivyo, kwa mujibu wa chapisho la Bild, Dortmund wana nia ya kujaribu kuwashawishi United msimu huu wa joto kwa kupunguza bei yao hadi £ 88m, ambayo inadhaniwa ni punguzo la £ 20m kwa hesabu yao ya awali..
Sancho, ambaye pia alikuwa akihusishwa na Chelsea na Liverpool, amefunga mabao 42 na kutoa asisti 56 katika mechi 124 za BVB tangu alipowasili kutoka Manchester City mwaka 2017.
Neptune’s Richies ni mchezo Unaokupa pesa chap chap huku ukiwa unaburudika kupitia Kasino ya Mtandaoni ndani ya Meridianbet.
Lydia Emmanuel Magoti
Duuh
Sania
Hiyo hatari
Adelta
Good news
Magdalena
Ata wakipunguza hakuna anae muhitaji kwa sasa
Rahma
Noma sana
Caroline
Kwani imekuwaje tena
Khadija
Habari njema
Dorophina
Haya sasa dau hilo hapo mezani kazi kwao
Venerose
Mmmh
Mwanahamisi
Hatari
Ernest Kimeru
Sancho kwasasa atauzwa kwa bei ya kawaida sana walishindwa kuchangamkia fursa wakati anawika
David Pere
Sancho, ambaye pia alikuwa akihusishwa na Chelsea na Liverpool, amefunga mabao 42 na kutoa asisti 56 katika mechi 124 za BVB tangu alipowasili kutoka Manchester City mwaka 2017.
Issa
United hawana shida nae
Hopemwaikuka
Sio mbaya
Sarah
Duuh
warda
Itakuwa poa sana aende Man U