Shirikisho la Mpira wa Miguu Tunisia (FTF) limemtangaza kocha raia wa Ufaransa, Herve Renard, kuwa Kocha Mkuu mpya wa timu ya taifa ya Tunisia kwa kipindi chote kilichobakia cha mashindano ya Dunia 2026, siku moja tu baada ya kumtimua Sabri Lamouchi.
Lamouchi aliondolewa kwenye nafasi hiyo Jumatatu kufuatia kipigo kizito cha mabao 5-1 ambacho Tunisia ilikumbana nacho dhidi ya Sweden katika mchezo wa Kundi uliofanyika Jumapili. Matokeo hayo yalionekana kuwa sababu kuu ya uamuzi wa shirikisho kufanya mabadiliko ya haraka benchi la ufundi.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Katika taarifa rasmi iliyotolewa na FTF, shirikisho hilo lilithibitisha uteuzi wa Renard na kueleza kuwa ameanza majukumu yake mara moja. “Shirikisho la Mpira wa Miguu Tunisia linatangaza kuteuliwa kwa Herve Renard kuiongoza timu ya taifa hadi mwishoni mwa Kombe la Dunia 2026,” ilisema sehemu ya taarifa hiyo.
Renard anafahamika kama mmoja wa makocha wenye uzoefu mkubwa katika soka la kimataifa, hususan barani Afrika, ambapo amewahi kupata mafanikio makubwa akiwa na timu mbalimbali za taifa. Uzoefu wake unatarajiwa kusaidia Tunisia kurejesha matumaini ya kufanya vizuri katika mechi zilizobakia za mashindano hayo.
Miongoni mwa mafanikio makubwa yaliyomjengea sifa Renard ni ushindi wa kushangaza wa Saudi Arabia dhidi ya Argentina katika Kombe la Dunia la mwaka 2022. Chini ya uongozi wake, Saudi Arabia iliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya mabingwa hao wa dunia, matokeo yaliyotikisa ulimwengu wa soka na kuthibitisha uwezo wake wa kuandaa timu kwa mechi kubwa.


