Alexander-Arnold Afurahia Kufanya Kazi na Mourinho Real Madrid

Beki wa Real Madrid, Trent Alexander-Arnold, amesema ni heshima na furaha kubwa kufanya kazi chini ya kocha mpya wa klabu hiyo, Jose Mourinho, akieleza kuwa amekuwa akimvutiwa kwa muda mrefu na anaamini ataiongoza timu hiyo kutwaa mataji katika msimu ujao.

Alexander-Arnold Afurahia Kufanya Kazi na Mourinho Real MadridMourinho alirejea kuinoa Real Madrid mwezi Juni kwa awamu yake ya pili, baada ya klabu hiyo kuwa na msimu usioridhisha ambapo ilikosa ubingwa wa LaLiga na kuondolewa katika hatua ya robo fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Ujio wake unaonekana kuleta matumaini mapya ndani ya kikosi cha miamba hiyo ya Hispania.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Akizungumza kuhusu kocha huyo, Alexander-Arnold alisema: “Nimekuwa nikimvutiwa Mourinho kwa muda mrefu. Nimewahi kucheza dhidi yake mara kadhaa, hivyo ni furaha kubwa kufanya kazi naye pamoja na benchi lake la ufundi. Kiwango cha nidhamu, mbinu na matarajio yake ni vya juu sana, jambo linalotupa hamasa ya kujifunza na kuendelea kuboresha kiwango chetu.”

Alexander-Arnold Afurahia Kufanya Kazi na Mourinho Real MadridBeki huyo wa kimataifa wa England aliongeza kuwa ana imani Mourinho atawasaidia wachezaji kuimarika zaidi. “Nina uhakika atatufundisha mambo mengi na kutusaidia kushinda mataji msimu huu. Sote tuna hamu ya kujifunza, kubadilika na kufikia mafanikio makubwa chini ya uongozi wake,” alisema.

Alexander-Arnold Afurahia Kufanya Kazi na Mourinho Real MadridAlexander-Arnold, aliyejiunga na Real Madrid akitokea Liverpool mwaka jana, alipitia msimu wa kwanza uliokumbwa na majeraha yaliyomzuia kupata nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza. Hata hivyo, kuondoka kwa Dani Carvajal mwezi Mei kumefungua nafasi kwake kuwa chaguo la kwanza katika beki ya kulia. Real Madrid itaanza kampeni yake ya LaLiga msimu wa 2026/27 kwa mchezo dhidi ya Espanyol utakaochezwa Agosti 22.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.