Amorim: Changamoto za Manchester United Zimemfanya Kuwa Kocha Bora AC Milan

Kocha mpya wa AC Milan, Rúben Amorim, amesema kipindi chake kigumu akiwa kocha wa Manchester United kimemsaidia kukua na kuwa kocha bora zaidi. Amorim alitoa kauli hiyo wakati akizungumza na waandishi wa habari kwa mara ya kwanza tangu ateuliwe kuiongoza Milan.

Amorim:  Changamoto za Manchester United Zimemfanya Kuwa Kocha Bora AC MilanKocha huyo raia wa Ureno ameonyesha furaha kujiunga na klabu hiyo yenye historia kubwa barani Ulaya na kusema anaamini mradi wa Milan unaendana na maono yake ya soka. “Tayari nahisi kama niko nyumbani. Tangu mazungumzo yetu ya kwanza, nilihisi hapa ni sehemu sahihi kwangu kutokana na maadili na misingi ya klabu,” alisema Amorim.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Amorim, mwenye umri wa miaka 41, amesema atajitahidi kujifunza lugha ya Kiitaliano haraka kama ishara ya heshima kwa mashabiki wa Milan. Pia amekiri kuwa makosa aliyoyafanya wakati akiwa Manchester United yamemjengea uzoefu mkubwa katika kazi yake ya ukocha. “Makosa niliyofanya huko nyuma yamenifanya kuwa kocha bora zaidi,” alisema.

Amorim:  Changamoto za Manchester United Zimemfanya Kuwa Kocha Bora AC MilanKatika mipango yake ya kujenga kikosi kipya cha Milan, Amorim amesisitiza umuhimu wa kusajili wachezaji wenye ubora akimtaja mshambuliaji Gonçalo Ramos kama aina ya mchezaji anayehitajika na timu hiyo. “Ramos ni mshambuliaji bora, bao lake kwenye michuano ya Dunia lilikuwa la kiwango cha juu. Ni aina ya mchezaji anayefaa kwenye timu tunayotaka kuijenga,” alisema.

Amorim:  Changamoto za Manchester United Zimemfanya Kuwa Kocha Bora AC MilanPia ameweka wazi kuwa anataka kiungo mkongwe Luka Modrić aendelee kuwa sehemu muhimu ya mipango yake msimu ujao. “Tunataka Modrić abaki. Tayari nimezungumza naye na kwangu bado ni mchezaji muhimu sana,” alisema Amorim. Mwenyekiti wa RedBird Capital Partners, Gerry Cardinale, amesema ujio wa Amorim ni mwanzo wa sura mpya kwa Milan baada ya klabu hiyo kushindwa kufuzu mashindano ya juu ya Ulaya msimu uliopita. “Tunapaswa kuirudisha AC Milan mahali inapostahili,” alisema Cardinale.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.