Beki wa kushoto wa Scotland, Andy Robertson, ameripotiwa kufikia makubaliano ya kujiunga na Tottenham Hotspur baada ya kuondoka rasmi ndani ya Liverpool mwishoni mwa wiki iliyopita. Taarifa zinaeleza kuwa nyota huyo yupo hatua za mwisho kukamilisha uhamisho wake kwenda Spurs.
Robertson alikuwa karibu kujiunga na Tottenham tangu dirisha la usajili la mwezi Januari, ambapo pande zote zilikuwa zimefikia makubaliano ya awali kabla ya dili hilo kuchelewa kukamilika. “Tottenham hawajawahi kuacha nia yao ya kumtaka Robertson na sasa wanaamini muda umefika wa kumpata,” kilieleza chanzo cha karibu na mazungumzo hayo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Wakati Spurs wakijiandaa kukamilisha dili hilo, mabingwa wa Italia, Juventus, walijaribu kuingilia kati kwa lengo la kuteka nyara uhamisho huo katika dakika za mwisho. Hata hivyo, Robertson ameonekana kuvutiwa zaidi na mradi wa Tottenham pamoja na nafasi ya kuendelea kucheza Ligi Kuu England.
Inaelezwa kuwa kocha Roberto De Zerbi ameidhinisha usajili huo na anaamini uzoefu wa Robertson utakuwa muhimu kwa kikosi hicho kuelekea msimu mpya wa mashindano. Beki huyo anatarajiwa kuongeza uimara pamoja na uzoefu mkubwa katika safu ya ulinzi ya Spurs.
“Makubaliano yapo katika hatua nzuri na kila kitu kinaelekea kukamilika hivi karibuni,” kiliongeza chanzo hicho huku mashabiki wa Tottenham wakisubiri kwa hamu tangazo rasmi la kuwasili kwa nyota huyo wa Scotland ndani ya klabu yao.


