Timu ya taifa ya Argentina imefuzu hatua ya robo fainali ya michuano ya Dunia 2026 baada ya kufanya mrejesho wa kuvutia na kuibuka na ushindi wa mabao 3-2 dhidi ya Misri katika mchezo wa hatua ya 16 bora uliochezwa kwenye Uwanja wa Mercedes-Benz mjini Atlanta. Mabingwa hao watetezi walitoka nyuma kwa mabao 2-0 huku zikiwa zimesalia dakika 11 kabla ya muda wa kawaida kumalizika na kufanikisha ushindi wa kihistoria.
Misri ilionekana kuwa njiani kuandika historia kupitia mabao ya Yasser Ibrahim na Mostafa Zico, lakini dakika ya 79 beki Cristian Romero alifunga bao la kwanza la Argentina kwa kichwa baada ya krosi safi ya Lionel Messi. Dakika nne baadaye, Messi aliisawazishia Argentina kwa shuti la volei lililokuwa bao lake la nane katika mashindano hayo, kabla ya Enzo Fernandez kufunga bao la ushindi katika dakika ya pili ya muda wa nyongeza.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Akizungumza baada ya ushindi huo, Fernandez alisema: “Kupitia nyakati kama hizi ni jambo la kumshukuru Mungu. Ni heshima kubwa kwangu kuwa sehemu ya kikosi hiki. Tunayo timu ya kipekee ambayo haikati tamaa hata inapokutana na changamoto. Siku zote tunabaki pamoja.”
Kwa upande wa Misri, mfungaji wa bao Mostafa Zico alieleza masikitiko yake kuhusu matukio ya kipindi cha pili, akidai kuwa maamuzi yaliyochukuliwa yalikuwa ya kutatanisha. “Tulicheza vizuri dhidi ya mabingwa wa dunia. Sijui nini kilitokea kipindi cha pili. Kulikuwa na mambo ya ajabu ambayo kila mtu aliona. Yalikuwa wazi kabisa,” alisema Zico, akirejea bao lililokataliwa na VAR pamoja na madai ya kunyimwa penalti.
Ushindi huo unaifanya Argentina kuendelea na safari ya kutetea taji lao la dunia, huku ikiwa mara nyingine ikinusurika baada ya pia kupata wakati mgumu dhidi ya Cape Verde katika hatua ya 32 bora. Kikosi hicho sasa kinaelekeza nguvu zake katika robo fainali, kikiongozwa na nahodha wake Lionel Messi ambaye ameendelea kuwa mhimili muhimu wa mafanikio ya timu hiyo.


