Kwa mujibu wa ripoti ya TEAMtalk, Bruno Guimarães anafuatiliwa na Arsenal. The Gunners wana nia ya kuimarisha kikosi chao cha kwanza kwa kumsajili kiungo mwenye uwezo wa kucheza nafasi mbalimbali katika dirisha hili la usajili, huku nyota huyo wa Newcastle United mwenye umri wa miaka 28 akiwa ndiye anayelengwa zaidi na klabu hiyo.

Ofa za awali kutoka klabu hiyo ya Kaskazini mwa London hazikuwa na thamani ya kutosha kukamilisha dili hilo, hivyo Arsenal iko tayari kurejea na ofa mpya ya pauni milioni 80 ili kupata saini ya kiungo huyo kutoka Amerika Kusini.
Hata hivyo, kwa mujibu wa TEAMtalk, Newcastle United itaendelea kupinga juhudi za Arsenal kumnasa Bruno Guimarães, huku klabu hiyo ikiwa imemuwekea bei ya juu ya “isiyowezekana” ya pauni milioni 90.




