Arsenal imeingia kwenye vita vikali vya usajili dhidi ya Paris Saint-Germain (PSG) katika harakati za kuwania saini ya winga wa Cologne, Said El Mala, ambaye ameibuka kuwa mmoja wa wachezaji waliovutia zaidi katika Bundesliga msimu uliopita.
Taarifa kutoka Ujerumani zinaeleza kuwa El Mala tayari ameweka wazi msimamo wake kuhusu mustakabali wake kwa kukataa uwezekano wa kujiunga na Brentford, licha ya klabu hiyo ya Ligi Kuu England kuwasilisha ofa rasmi kabla ya mwisho wa msimu. “Mchezaji huyo hana nia ya kujiunga na Brentford kwa sasa, huku akivutiwa zaidi na miradi ya klabu kubwa zinazoshiriki michuano ya Ulaya,” zimeeleza taarifa hizo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Arsenal na PSG sasa zinaonekana kuwa mbele katika mbio za kuipata saini ya nyota huyo, ambaye ameonyesha kiwango bora kilichomfanya kuwa miongoni mwa masupastaa waliotikisa Bundesliga msimu uliopita. “El Mala amevutia macho ya vigogo kadhaa wa Ulaya kutokana na uwezo wake wa kushambulia, kasi na ubunifu akiwa uwanjani,” imeelezwa.
Wakati huo huo, El Mala tayari ameijulisha Cologne kwamba hana mpango wa kuendelea kuitumikia klabu hiyo msimu ujao. “Nataka changamoto mpya katika hatua inayofuata ya maisha yangu ya soka,” inaelezwa kuwa ni sehemu ya ujumbe alioufikisha kwa viongozi wa timu hiyo.
Licha ya nia yake ya kuondoka, Cologne bado ipo kwenye nafasi nzuri ya kujadiliana kutokana na mkataba wa mchezaji huyo kuendelea hadi Juni 30, 2030. Hali hiyo inamaanisha klabu yoyote inayohitaji huduma zake italazimika kuandaa dau kubwa ili kuishawishi Cologne kumruhusu nyota huyo kuondoka mapema.


