Arsenal inaripotiwa kufikia makubaliano na Club Brugge ya Ubelgiji kumsajili winga wa kimataifa wa Ugiriki, Christos Tzolis, kwa ada inayokadiriwa kufikia euro milioni 40. Kwa mujibu wa vyanzo mbalimbali, ikiwemo mwandishi wa The Athletic David Ornstein, makubaliano hayo yanatarajiwa kuweka historia kama mauzo makubwa zaidi kuwahi kufanywa na Club Brugge.
Tzolis mwenye umri wa miaka 24 aling’ara msimu uliopita akiwa na Club Brugge baada ya kufunga mabao 17 na kutoa pasi 23 za mabao katika michezo 37 ya Ligi Kuu ya Ubelgiji, akichangia kwa kiwango kikubwa mafanikio ya klabu hiyo kutwaa ubingwa. Arsenal inaamini kiwango chake kitaiimarisha safu ya ushambuliaji kuelekea msimu mpya.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Iwapo uhamisho huo utakamilika, euro milioni 40 zitakuwa ada kubwa zaidi kuwahi kupokelewa na Club Brugge kwa mauzo ya mchezaji, zikivunja rekodi ya awali ya euro milioni 37.5 iliyowekwa mwaka 2021 baada ya Charles De Ketelaere kuuzwa. Taarifa zinaeleza kuwa Tzolis anatarajiwa kusaini mkataba wa angalau miaka mitano kuitumikia Arsenal.
Safari ya Tzolis katika soka la kulipwa ilianza akiwa PAOK ya Ugiriki kabla ya kuhamia Norwich City mwaka 2021. Baadaye alicheza kwa mkopo FC Twente ya Uholanzi, kisha akajiunga moja kwa moja na Fortuna Düsseldorf mwaka 2024 kwa euro milioni 3.5. Hata hivyo, ndani ya wiki moja tu Club Brugge ilimsajili kwa euro milioni 6.5, hatua iliyogeuka kuwa moja ya biashara zenye faida kubwa kwa klabu hiyo.
Katika kipindi chake akiwa Club Brugge, Tzolis alicheza mechi 108, akifunga mabao 43 na kutoa pasi 47 za mabao. Akinukuliwa na taarifa mbalimbali za uhamisho, “Arsenal na Club Brugge wamekubaliana ada ya euro milioni 40, huku Tzolis akitarajiwa kusaini mkataba wa angalau miaka mitano jijini London Kaskazini,” hatua inayomkaribisha winga huyo kuwa sehemu ya kikosi cha Mikel Arteta kwa msimu ujao.


