Bao pekee lililofungwa na Kai Havertz limeipa ushindi muhimu Arsenal F.C. na kuiweka katika nafasi nzuri ya kutwaa ubingwa wa Premier League msimu wa 2025/2026.
Ushindi huo umeifanya Arsenal kufikisha pointi 82 kileleni mwa msimamo wa ligi, huku ikipewa nafasi kubwa ya kutwaa taji hilo ikiwa imesalia na mchezo mmoja pekee kabla ya msimu kumalizika.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Washika Mitutu hao wa London wanatarajiwa kucheza mchezo wao wa mwisho dhidi ya Crystal Palace F.C. Mei 24, 2026, ambapo ushindi utawafanya wafikishe pointi 85 ambazo haziwezi kufikiwa na timu yoyote nyingine msimu huu.
Hata hivyo, Arsenal inaweza kutangazwa mabingwa mapema iwapo Manchester City F.C. itashindwa kupata ushindi dhidi ya AFC Bournemouth katika mchezo wao wa leo usiku wa Jumanne Mei 19, 2026.
“Arsenal wameonyesha uthabiti mkubwa msimu huu na sasa wanahitaji ushindi mmoja pekee kuhakikisha wanatwaa ubingwa wa Premier League,” zimeeleza taarifa za ligi hiyo.


