Kocha mkuu wa Arsenal FC, Mikel Arteta, amethibitisha kuwa nahodha wa timu hiyo Martin Ødegaard hatakuwepo katika mchezo wa kwanza wa hatua ya 16 bora ya UEFA Champions League dhidi ya Bayer 04 Leverkusen utakaochezwa leo Jumatano. Hata hivyo, Arteta ametoa taarifa njema kwa kuthibitisha kuwa beki wa kati William Saliba yupo fiti na tayari kucheza katika mchezo huo muhimu.

William Saliba alikosa michezo miwili iliyopita ya Arsenal katika mashindano yote kutokana na jeraha la kifundo cha mguu, lakini sasa amepona na anatarajiwa kurejea kuimarisha safu ya ulinzi ya timu hiyo. Kurejea kwake kunampa nafuu Arteta kuelekea pambano hilo gumu la Ulaya.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Hata hivyo, kutokuwepo kwa Martin Ødegaard kunaacha pengo kubwa katika eneo la kiungo kwa Arsenal, hasa upande wa ubunifu wa mashambulizi. Arteta pia alieleza kuwa Riccardo Calafiori na Leandro Trossard wanaweza kuwepo kwenye kikosi, ingawa uamuzi wa mwisho utafanyika karibu na muda wa mchezo.

Aidha, Arteta alithibitisha kuwa wachezaji muhimu akiwemo Gabriel Magalhães, Declan Rice na Martín Zubimendi wote wapo tayari kwa mchezo huo. Upatikanaji wao unaipa Arsenal nguvu zaidi katika kikosi kuelekea mechi hiyo muhimu ya Ulaya.
Arsenal iliondolewa katika hatua ya nusu fainali ya Ligi ya Mabingwa msimu uliopita, na hivyo kushindwa kufikia ndoto ya kutwaa taji hilo kwa mara ya kwanza katika historia ya klabu. Akizungumzia uzoefu huo, Arteta alisema timu yake imejifunza mambo mengi kutokana na tukio hilo.
“Ndiyo, unajifunza mambo uliyofanya vizuri na pia yale unayopaswa kuboresha, Huu ni mpira wa miguu na lazima uonyeshe uwezo wako kesho usiku. Ligi ya Mabingwa inahusu siku ya mchezo na ndani ya siku hiyo kuna nyakati muhimu.”

Arsenal inaingia katika mchezo huo ikiwa kwenye kiwango kizuri baada ya kuifunga Mansfield Town FC mabao 2-1 mwishoni mwa wiki na kufuzu hatua ya robo fainali ya FA Cup. Ushindi huo umeibua mjadala kuhusu uwezekano wa timu hiyo kutwaa mataji manne msimu huu, huku Arsenal pia ikiongoza msimamo wa EPL.

