Mikel Arteta amesema kwamba “hakuna tatizo” kati ya wachezaji David Luiz na Dani Ceballos baada ya wawili hao kuripotiwa kutofautiana wakati wa mazoezi.
Meneja wa Arsenal Arteta amesisitiza “hakuna kitu kilichotokea” katika viwanja vya mazoezi vya Colney na aliamua kuipiga chini stori hiyo.
“Mazoezi ni ya ushindani sana mambo kama haya hutokea mara kwa mara,” Arteta aliongea nawaandishi siku ya Ijumaa.
“Na mambo hayo yaliisha haraka sana ndani ya timu, hakuna zaidi ya kuongea hakuna tatizo kati yao.
Alipoulizwa kama alishuhudia mkwaruzano huo, arteta aliongeza: “Nilipata picha mbaya nilikuwa kwa mbali ndiyo maana tunafanya mazoezi bila uwepo wa watu wengine.
Arteta alikabiliana na ishu nyingine ya kinidhamu baada ya mchezaji raia wa Brazil Willian kuweka picha yake katika mtandao Instagram akiwa Dubai.
Sheria za serikali ya United Kingdom haziruhusu mtu kusafiri kwenda taifa lingine isipokuwa kwa sababu maalumwakati huu wa kukabiliana na COVID-19.
Willian alijiunga na Arsenal akitokea klabu ya Chelsea kwa uhamisho huru lakini amekuwa akipambana kujitafuta kuwa kwenye fomu nzuri akiwa hajafanikiwa kufunga goli na kutoa asisti mbili katika michezo saba ya Premier League msimu huu.
Arteta alipuuza kuongelea swala la Willian kama amekiuka utaratibu wa klabu kwa kusafiri mapaka Dubai na je atatemwa kwenye mchezo wa Jumapili dhidi Leeds United.
Hauhitaji kuwaza linapokuja suala la ubashiri na odds kubwa. Bashiri na Meridianbet ukiwa popote ufurahie ushindi mkubwa katika michezo mbalimbali na hadi milioni 16 kwenye michezo ya kasino.
Adelta
Ni vizuri Kama hamna tofauti
Hopemwaikuka
Afadhali ikiwa hvyo
Povel
Nice information
Sabrina
Basi sawa inapendeza sana
Angelina
Niceupdate
magdalena
kama wamemaliza tofauti zao hakuna shida maisha ya soka yaendelee
Fatina mfingi
Kam wamemaliza tofauti Ni jambo zuri
Sauda
Bora zaidi
zeiyana
Arteta ni kocha hanayejielewa yeye kama yeye hatayamliza ukingalia ni kweli kila sehemu wanapo kutana watu tofauti tofauti lazima mambo kama hayo yatokee
Lydia Emmanuel Magoti
Vizuri Sana Kama hipo hivyo
Caroline
Mpira hautaki ugomvi
aisha
Ni jambo la maana
Saupha mohamed
IPO vizuri
Ester jackson
Asante kwa taarifa
warda
Ni vizuri kuelewana