Licha ya Barcelona kutwaa ubingwa wa La Liga msimu huu, ndani ya klabu hakuna dalili ya kusherehekea wala kuridhika. Kocha Hansi Flick na kikosi chake sasa wameweka lengo jipya kubwa, kubadilisha msimu huu kuwa wa kihistoria kwa kuvunja rekodi kadhaa ambazo bado zipo mbele yao.

Kwa sasa Barcelona wana pointi 91 na bado wana mechi tatu mkononi. Lengo lao kubwa ni kufikisha pointi 100, hatua ambayo imefikiwa mara chache sana katika historia ya La Liga. Hii ni changamoto kubwa inayowataka washinde mechi zote zilizosalia ili kujiweka kwenye orodha ya klabu za kipekee zaidi Ulaya.
Mbali na hilo, Barcelona pia wanaendelea na mfululizo kufunga katika mechi 56 mfululizo za La Liga. Rekodi ya kihistoria ni mechi 63 mfululizo, na hivyo kikosi cha Flick kiko karibu sana kuandika ukurasa mpya wa mafanikio ya mashambulizi ya klabu hiyo.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Kwa upande wa ubora wa matokeo, Barcelona pia wako kwenye mfululizo wa ushindi ambao unaweza kufikia mechi 11 mfululizo za ligi, ingawa bado wako mbali na rekodi ya klabu ya ushindi 16 mfululizo iliyowekwa enzi za Pep Guardiola.

Ndani ya Camp Nou, hali ya ushindi inaendelea hata nyumbani ambapo Barcelona wako kwenye safari ya kushinda mechi 18 mfululizo. Zaidi ya hapo, ushindi wao wa El Clásico umewafanya wafikishe ushindi 106 sawa na Real Madrid katika historia ya mapambano hayo, huku pia wakionekana kuwa na nafasi ya kuongeza pengo kubwa zaidi la pointi dhidi ya wapinzani wao wa jadi.


