Kiungo nyota wa PSV Eindhoven, Ismael Saibari, anatajwa kuwa mbioni kujiunga na Bayern Munich baada ya klabu hizo mbili kufikia makubaliano ya uhamisho wake. Taarifa kutoka kwa vyanzo mbalimbali vya karibu na mchakato huo zinaeleza kuwa nyota huyo wa kimataifa wa Morocco atasaini mkataba wa miaka mitano na mabingwa hao wa Ujerumani.
Makubaliano hayo yanaripotiwa kugharimu hadi euro milioni 55, ambapo euro milioni 50 ni ada ya msingi huku kiasi kilichobaki kikitegemea bonasi mbalimbali. Endapo bonasi hizo zitafikiwa, uhamisho huo utaweka rekodi mpya ya mauzo makubwa zaidi katika historia ya PSV. “Bayern Munich wamefikia makubaliano na PSV kwa ajili ya uhamisho wa Ismael Saibari,” zimeeleza taarifa za ndani ya dili hilo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Bayern walielekeza nguvu zao kwa Saibari baada ya kushindikana kumpata winga wa Newcastle United, Anthony Gordon. Kocha Vincent Kompany aliaminika kuvutiwa na kiwango cha nyota huyo baada ya kuwa na msimu bora akiwa na PSV, ambao walitwaa ubingwa wa Eredivisie kwa tofauti ya alama 19 dhidi ya wapinzani wao wa karibu.
Saibari alitangazwa kuwa Mchezaji Bora wa Msimu wa Eredivisie baada ya kufunga mabao 15 na kutoa pasi nane za mabao katika michezo 27 ya ligi. Kiungo huyo mwenye asili ya Hispania na anayeiwakilisha Morocco kimataifa ameendelea kuonyesha maendeleo makubwa tangu alipojiunga na akademi ya PSV mwaka 2020 akitokea KRC Genk.
Katika jumla ya mechi 142 alizoichezea PSV katika mashindano yote, Saibari amefunga mabao 42 na kutoa pasi za mabao 28. Endapo dili hilo litakamilika rasmi, atakuwa mchezaji wa kwanza katika historia ya PSV kujiunga moja kwa moja na Bayern Munich akiwa anatoka kwa mabingwa watetezi wa Eredivisie, hatua inayotarajiwa kuandika ukurasa mpya katika historia ya klabu zote mbili.


