Mkurugenzi wa michezo wa Bayern Munich, Christoph Freund, amesema klabu ya Liverpool inapaswa kuachana na ndoto za kumsajili winga Michael Olise katika dirisha hili la usajili.
Olise, mwenye umri wa miaka 24, amekuwa akihusishwa kwa karibu na Liverpool ambayo inaendelea kutafuta mbadala wa muda mrefu wa mshambuliaji Mohamed Salah. Hata hivyo, Bayern Munich imeweka wazi kuwa nyota huyo hayupo sokoni kwa sasa.
ligi kuu ya uingereza, ligi kuu England, odds za epl, mechi za ligi kuu uingereza, bashiri mechi za EPL, beti mechi za premier league, odds za ligi kuu England, odds za premier league
Akizungumza kuhusu mustakabali wa mchezaji huyo, Freund alinukuliwa akisema, “Michael Olise ataendelea kuwa mchezaji wa Bayern Munich msimu ujao. Hatuna mpango wa kumuuza katika dirisha hili la usajili.” Kauli hiyo imeonekana kama jibu la moja kwa moja kwa uvumi unaoihusisha Liverpool na mchezaji huyo.
Kwa upande mwingine, Liverpool imekuwa ikitafuta kuongeza nguvu katika safu ya ushambuliaji, hasa upande wa winga, huku ikitathmini chaguo mbalimbali kabla ya kuanza kwa msimu mpya wa Premier League.
Licha ya taarifa hizo kuendelea kusambaa Ulaya, Bayern inaonekana kuwa na msimamo thabiti kuhusu Olise. Freund alisisitiza tena kwamba, “Tunamwona Olise kama sehemu muhimu ya mradi wetu wa baadaye, hivyo hakuna mazungumzo ya kumruhusu aondoke kwa sasa.” Kauli hiyo inaashiria kuwa Liverpool italazimika kuelekeza macho kwa malengo mengine ikiwa bado inahitaji winga mpya kabla ya kufungwa kwa dirisha la usajili.


