Kiungo wa zamani wa Real Madrid na Manchester United, Casemiro, amefichua kuwa jina lake la kweli ni Carlos Henrique Casimero, huku jina la Casemiro linalotambulika duniani kote likitokana na kosa la tahajia lililotokea alipokuwa akichezea São Paulo nchini Brazil.
Nyota huyo wa Brazil amesema mkanganyiko huo ulianza baada ya klabu yake ya zamani kuandika vibaya jina lake kwenye jezi kwa kubadilisha herufi “I” na “E”. Licha ya kugundua kosa hilo, hakulirekebisha kwa kuwa aliamini lilimletea bahati baada ya kucheza vizuri katika mechi hiyo.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
“Jina langu halisi ni Carlos Henrique Casimero, lakini kosa la tahajia kwenye jezi lilifanya nitambulike kama Casemiro. Baada ya kucheza vizuri siku hiyo, niliamua kuliacha liendelee,” amesema kiungo huyo wa Brazil.
Tangu wakati huo, jina la Casemiro likawa alama yake rasmi katika soka la kimataifa. Akiwa na jina hilo, amefanikiwa kutwaa mataji makubwa akiwa Real Madrid, kuichezea Manchester United na kuwa mmoja wa wachezaji muhimu wa timu ya taifa ya Brazil.
“Kilichoanza kama kosa la herufi moja kiligeuka kuwa sehemu ya utambulisho wangu wa soka na kikanisindikiza katika mafanikio yote niliyoyapata,” ameongeza Casemiro.


