Chelsea Wapo Tayari Kumuuza Garnacho Iwapo Ofa Kubwa Itawasilishwa

Mustakabali wa winga wa Argentina, Alejandro Garnacho, ndani ya Chelsea unaonekana kuwa wa mashaka baada ya taarifa kuonyesha kuwa klabu hiyo ipo tayari kusikiliza ofa nono kwa ajili ya mchezaji huyo katika dirisha la usajili la majira ya joto.

Chelsea Wapo Tayari Kumuuza Garnacho Iwapo Ofa Kubwa ItawasilishwaGarnacho mwenye umri wa miaka 21 alijiunga na Chelsea akitokea Manchester United mwaka jana kwa ada inayokadiriwa kufikia pauni milioni 40. Hata hivyo, maisha yake ndani ya Stamford Bridge hayajawa rahisi kwani alishindwa kujihakikishia nafasi ya kudumu katika kikosi cha kwanza.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Katika msimu uliopita, Garnacho alianza michezo 14 ya Ligi Kuu England na michezo mitatu ya Ligi ya Mabingwa Ulaya. Akiunganisha mechi alizoanza na zile alizoingia akitokea benchi, alicheza mara 33 kwenye mashindano hayo mawili akifunga mabao mawili na kutoa pasi nne za mabao.

Chelsea Wapo Tayari Kumuuza Garnacho Iwapo Ofa Kubwa Itawasilishwa“Chelsea hawamlazimishi Garnacho kuondoka, lakini wako tayari kupokea ofa kubwa endapo itawasilishwa,” chanzo kilicho karibu na klabu hiyo kimenukuliwa kikisema, huku ikielezwa kuwa viongozi wa timu hiyo tayari wanafanya maandalizi ya kutafuta winga mwingine wa kiwango cha juu kwa ajili ya upande wa kushoto wa safu ya ushambuliaji.

Chelsea Wapo Tayari Kumuuza Garnacho Iwapo Ofa Kubwa ItawasilishwaMabadiliko makubwa yanatarajiwa Chelsea baada ya kuwasili kwa kocha mpya Xabi Alonso. Ripoti zinaeleza kuwa Garnacho huenda asiwe sehemu ya mipango ya muda mrefu ya kocha huyo, huku pia viungo Enzo Fernandez na kipa Robert Sanchez wakitajwa miongoni mwa nyota wanaoweza kuondoka iwapo ofa zinazovutia zitawasilishwa.

Chelsea Wapo Tayari Kumuuza Garnacho Iwapo Ofa Kubwa Itawasilishwa“Serie A inaweza kuwa kituo kinachofuata kwa Garnacho iwapo ataondoka Chelsea,” vyanzo hivyo vimeeleza. Klabu kadhaa za Italia zinaaminika kufuatilia kwa karibu hali ya nyota huyo wa Argentina, huku Chelsea ikionekana kuwa tayari kufanya mabadiliko makubwa ya kikosi katika harakati za kurejea kwenye ushindani wa juu baada ya kumaliza nafasi ya 10 kwenye msimamo wa Ligi Kuu msimu uliopita.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.