Baada ya Kipigo cha jana kwa Spurs, Kocha wa timu hiyo Antonio Conte amelenga Arsenal kwa kuwakumbusha ni nani atacheza Ligi ya Mabingwa wiki hii.

Kocha huyo wa Tottenham alikasirishwa sana baada ya kuona timu yake ikichapwa mabao 3-1 na Arsenal kwenye mchezo wa kaskazini mwa London.

Thomas Partey aliipatia timu ya Mikel Arteta bao la kuongoza, kabla ya Harry Kane kusawazisha mchezo huo kwa mkwaju wa penalti kabla ya mapumziko.

 

Conte: Sisi Tunacheza UCL

Gabriel Jesus na Granit Xhaka pia waliifungia Arsenal bao lao, kabla ya kadi nyekundu kwa Emerson Royal kumaliza mchezo ambao ulikuwa mbaya sana kwa Spurs kwenye Uwanja wa Emirates.

Huku akiwa amekatishwa tamaa na juhudi za timu yake, Conte hakuweza kujizuia kuwakumbusha wapinzani wake jinsi mwisho wa msimu uliopita wa Ligi Kuu ulivyofanyika, huku Tottenham wakiwazamisha washika mtutu, hadi kumaliza katika nne bora katika wiki ya mwisho ya msimu.

 

Conte: Sisi Tunacheza UCL

Akizungumza baada ya mechi Conte alisema: “Tulijaribu kufanya tuwezavyo na tunajaribu kuimarika na kwenda mchezo baada ya mchezo na kuona nini kitatokea mwishoni mwa msimu.

“Kwa hakika, lazima tujaribu kuimarika lakini narudia maoni yangu kwamba Tottenham ndio wameanza kujaribu na kuwa washindani. Lazima tuendelee kufanya kazi na kuboresha hatua kwa hatua kwa unyenyekevu na si kwa kudhania.

“Kuna neno moja tu kwetu na hilo ni kufanya kazi. Tunahitaji kusonga mbele na kucheza mchezo katika Ligi ya Mabingwa.

 

Conte: Sisi Tunacheza UCL

“Usisahau kuwa msimu uliopita tulikuwa nyuma ya Arsenal kukiwa na michezo miwili iliyobaki, walikuwa na pointi nne mbele yetu na sasa tunacheza Ligi ya Mabingwa na wanacheza UEFA [Europa League] na hivyo tunahitaji juhudi kubwa ili mbele katika shindano hili.”

JIBU

Tafadhali andika maoni yako
Tafadhali andika jina lako hapa