Dani Alves Hajafanyiwa Maamuzi Barcelona!

Kinyume na ripoti za hivi punde zinazodai kwamba Dani Alves atapewa mkataba mpya na Barcelona ambao utadumu hadi msimu ujao, Diario AS wameripoti kwamba mustakabali wa beki huyo wa kulia wa Brazil bado haujaamuliwa na klabu ya Barcelona.

Makocha na uongozi wa michezo wa klabu wanapendelea kusubiri hadi mwisho wa msimu kabla ya kufanya uamuzi, sababu zinatajwa kuwa ni kwamba bado kuna sintofahamu juu ya mipango ya uhamisho wa Barcelona msimu huu wa joto.

Dani Alves Hajafanyiwa Maamuzi Barcelona!
Dani Alves


Ikiwa Barca watawapata Cesar Azpilicueta na Noussair Mazraoui, Dani Alves atakuwa na wakati mgumu kupata namba, hasa ikiwa Sergino Dest pia atasalia Camp Nou.

Lakini hisia bado ni chanya linapokuja suala la mkongwe huyo wa Brazil. Dani Alves amekuwa sehemu muhimu ya chumba cha kubadilishia cha Barcelona ndani na nje ya uwanja.

Usajili wake kutoka Sao Paulo wakati wa dirisha la uhamisho wa Januari umekuwa wa mafanikio, lakini uamuzi wa mwisho kuhusu mustakabali wake bado haujafanywa.


VUNA MKWANJA NA SHINDANO LA EVOPLAY SPRING AWEKING

Mchongo mpya mjini ni Shindano la Evoplay Spring Aweking katika kasino maridhawa za meridianbettz. Pata mgao wako wa TSh 25,000,000  katika michezo kibao ya kasino na sloti ziliyochaguliwa kushiriki.

tetesi, Tetesi za Soka Barani Ulaya., Meridianbet

SOMA ZAIDI HAPA

Acha ujumbe