De la Fuente Afichua Siri ya Yamal, Asema Moto Wake Halisi Bado Haujawaka

Kocha wa Hispania, Luis de la Fuente, amesema bado dunia haijaiona kiwango bora kabisa cha nyota kijana Lamine Yamal, akiamini mchezaji huyo ataonyesha uwezo wake kamili kadri michuano ya Dunia 2026 linavyoendelea. Kauli hiyo ameitoa wakati Hispania ikijiandaa kuvaana na Ubelgiji katika mchezo wa robo fainali utakaochezwa jijini Los Angeles.

De la Fuente amesema licha ya Yamal kuwa sehemu muhimu ya kikosi chake, bado hajafikia kiwango cha kushambulia ambacho mashabiki wamezoea kukiona. Tunajua bado hatujaiona toleo bora kabisa la Lamine kwenye mashindano haya. Bado hajafikia kiwango cha ushambuliaji tunachokifahamu kutoka kwake, lakini tunaamini muda wake unakuja,” alisema kocha huyo.

Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa

Nyota huyo mwenye umri wa miaka 18 ameifungia Hispania bao moja pekee bila kutoa pasi ya mabao kwenye michuano hiyo, huku akitajwa kuwa aliwasili Marekani akiwa bado anarejea kutoka kwenye majeraha ya mwishoni mwa msimu. Hata hivyo, De la Fuente alisisitiza kuwa Yamal ameendelea kuwatesa mabeki wa timu pinzani, akitolea mfano mchezo dhidi ya Ureno ambapo alisema beki Nuno Mendes alilazimika kutoka nje kutokana na presha kubwa aliyowekewa na Yamal. “Alimlazimisha mpinzani wake kufanya kazi kubwa kiasi cha kuumia. Huo unaonyesha mchango wake uwanjani,” alieleza.

De la Fuente Afichua Siri ya Yamal, Asema Moto Wake Halisi Bado HaujawakaKocha huyo ameongeza kuwa changamoto ambazo Yamal amekutana nazo kwenye mashindano ya Dunia zimemjengea ukomavu mkubwa wa kisoka. “Hahitaji motisha ya ziada. Wakati mwingine tunalazimika kumpunguza kasi kwa sababu ana hamasa kubwa na anataka kufanya mengi kwa wakati mmoja. Amejifunza na amekomaa zaidi kupitia mashindano haya,” alisema.

De la Fuente Afichua Siri ya Yamal, Asema Moto Wake Halisi Bado HaujawakaHispania bado haijaruhusu kufungwa bao lolote kwenye michuano ya Dunia 2026, lakini sasa itakutana na Ubelgiji iliyotikisa kwa kuifunga Marekani mabao 4-0 hatua iliyopita. De la Fuente anaamini robo fainali hiyo inaweza kuwa jukwaa la Yamal kurejea kwenye ubora wake wa kushambulia. “Nina uhakika atafanya makubwa katika eneo la ushambuliaji. Ana kipaji cha kipekee na naamini bado mengi mazuri kutoka kwake yanakuja,” alihitimisha.

Acha ujumbe

Meridianbet
Privacy Overview

This website uses cookies so that we can provide you with the best user experience possible. Cookie information is stored in your browser and performs functions such as recognising you when you return to our website and helping our team to understand which sections of the website you find most interesting and useful.