Kocha mkuu wa timu ya taifa ya, Luis de la Fuente, amewataka mashabiki na wadau wa soka kuwa watulivu baada ya timu yake kutoka sare ya bila kufungana (0-0) dhidi ya Cape Verde katika mchezo wao wa kwanza wa Kundi H wa mashindano ya Dunia 2026.
Licha ya mabingwa hao wa Ulaya kutawala umiliki wa mpira kwa kiasi kikubwa na kutengeneza nafasi kadhaa za kufunga, walishindwa kuzitumia ipasavyo huku Cape Verde ikionyesha uimara mkubwa wa kujilinda na kuwazuia Wahispania kupata bao.
Bila kusahau meridianbet ndio wakali wa ODDS KUBWA, Machaguo zaidi ya 1000 na kila kitu ukitakacho. Bashiri kijanja hapa
Akizungumza baada ya mchezo huo, De la Fuente alikiri kuwa timu yake ilikosa umakini na ubunifu wa mwisho mbele ya lango, akisisitiza kuwa wakati mwingine matokeo ya soka huamuliwa na mambo madogo ambayo hayawezi kudhibitiwa.
“Suluhisho ni kuendelea kusisitiza falsafa yetu ya mchezo na kuboresha umaliziaji. Tulitengeneza nafasi nyingi lakini hatukuwa na ubora wa mwisho unaohitajika katika mechi za aina hii,” alisema De la Fuente.
Kocha huyo pia aliisifu Cape Verde kwa mpangilio wake mzuri wa kiuchezaji, akieleza kuwa walijilinda kwa wachezaji wengi nyuma jambo lililowafanya kuwa wagumu kuvunjwa licha ya presha kubwa kutoka Hispania.
“Ni timu iliyopangwa vizuri sana. Walicheza kwa kujilinda kwa kina na hali hiyo ilifanya iwe vigumu kupata nafasi wazi. Hata hivyo tulitengeneza nafasi kadhaa, lakini mpira haukutaka kuingia wavuni,” aliongeza.
Matokeo hayo yanaifanya Hispania kuanza kampeni yao ya mashindano hayo kwa pointi moja, huku De la Fuente akisisitiza kuwa bado wana muda wa kurekebisha makosa na kurejea kwenye kiwango chao katika mechi zijazo za kundi hilo.


